Header Ads

Habari kuu leo Jumatano

      Habari kuu leo Jumatano

Wachanganuzi wanasema kuwa, Korea Kaskazini imepiga hatua katika uundaji zana za kinuklia
Mkurugenzi mkuu wa idara ya upelelezi nchini Marekani, James Clapper, amesema kuwa sera ya kujaribu kuishawishi Korea Kaskazini, kuachana na mpango wake wa kuunda zana za kinuklia, bila shaka ni kupoteza muda bure. Katika hotuba, amesema kuwa la muhimu kwa Marekani kufanya ni kuidhibiti taifa hilo ili lisiendelee na azma yake ya kuunda zana hizo za kitonoradi.
Bunge la Congress nchini Venezuela, limepiga kura ya kuanzisha kesi ya kisiasa dhidi ya Rais wa chama cha Kisosiolisti, Nicolas Maduro, na kusababisha taharuki zaidi kati ya serikali na bunge la kitaifa, linaloongozwa na wanasiasa wa upinzani. Bunge hilo la Congress, linamtuhumu Bwana Maduro, kwa ukiukaji wa demokrasia.

 Rais Nichola Maduro



Kampuni ya Apple imetangaza kuwa imeuza zaidi ya simu milioni 45, muundo wa i-Phone, katika kipindi kilichopita cha robo mwaka ya utendakazi nchini Marekani. Hiyo ni zaidi ya ilivyotarajiwa, lakini ni robo ya tatu mtawalio ya uuzaji duni wa rununu ya smartphone.
Serikali ya Gambia, inasema kwamba itajiondoa mara moja, kutoka mahakama ya kimataifa ya makosa ya jinai-ICC, huku ikiilaumu kwa kuwahukumu waafrika pekee. Uamuzi huo unafuatia ule wa Afrika Kusini na Burundi, ya kujiondoa kutoka katika mahakama hiyo, iliyoko The Hague nchini Uholanzi. Rais Yahya Jammeh, ametawala Gambia tangu alipochukua uongozi kwa njia ya mapinduzi, mwaka 1994. Muendesha mashtaka mkuu wa sasa wa ICC, Fatou Bensouda ni mzaliwa wa Gambia.


Rais wa Gambia, Yahya Jammeh



Hakimu wa Mahakama Kuu nchini Marekani, ameidhinisha zaidi ya dola bilioni 15, dhidi ya kampuni ya uundaji magari- VolksVagen, kuhusiana na kashfa ya utoaji moshi chafu ya diezel. Zaidi ya wamiliki nusu milioni wa magari ya VolksVagen, wanaweza kuuza tena magari yao au kuyareshesha, ili kurekebishwa.
Mgombea kiti cha Urais wa chama cha Republican Nchini Marekani Donald Trump, amesema kuwa sera za kigeni za mpinzani wake Bi Hillary Clinton kuhusiana na Syria, itasababisha vita kuu ya tatu ya Dunia. Bwana Trump, amesema Marekani inafaa kulenga kuliangamiza kundi la Islamic State, badala ya kujaribu kumshawishi Rais wa Syria, Bashar al-Assad, kujiuzulu.


Vita Nchini Syria

Na tuzo ya vitabu ya The Man Booker, limenyakuliwa na Mwaandishi vitabu mmarekani Paul Beatty, kwa riwaya yake ya The Sell-Out. Kitabu hicho kinaangazia kinaya ya ubaguzi wa rangi.

No comments