Header Ads

Mauaji ya vikongwe,umasikini,ushirikishwaji hafifu katika Nyanja mbalimbali ni baadhi ya changamoto zinazowakabili wazee

Mauaji ya vikongwe,umasikini,ushirikishwaji hafifu katika Nyanja mbalimbali ni baadhi ya changamoto zinazowakabili wazee

Image result for MKUU WA WILAYA SHINYANGA



Akizungumza katika mkutano uliohusisha waandishi wa habari na viongozi  baraza la  wazee wa wilaya ya Shinyanga,Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga JOSEPHINE MATIRO ametaja changamoto mbalimbali zinazowakabili kundi hilo ikiwemo mauaji
Mheshimiwa MATIRO amesema mauaji  hasa kwa wanawake yameendelea kuwanyima amani wazee na kuwaweka katika hali ya wasiwasi.

               
Mmoja wa viongozi katika baraza la wazee BONIFAS BOAZ ameeleza adha wanazokumbana nazo wazee wakati wa upatikanaji wa huduma katika baadhi ya vituo vya afya.
                                      
Amesema serikali ipo tayari kuweka mazingira rafiki kwa wazee ikiwa ni Pamoja na kuweka  mikakati ya  kukabiliana na changamoto hizo sambamba  na kuwakamata watuhumiwa wanaojihusisha na mauaji ya vikongwe.
Amesema wazee ni hazina na kwamba  serikali inatambua mchango wao katika ujenzi wa taifa la Tanzania


No comments