Header Ads

Takukuru mkoani tabora imeokoa milioni miamoja lakisaba elfusitini na themani na sita



Takukuru mkoani tabora imeokoa   milioni miamoja lakisaba elfusitini na themani na sita  kutoka kwa wadau mbalimbali
Akizungumza na waandishi wa habari leo katika ukumbi wa takukuru  mkurungezi wa takukuru mkao watabora MOGASA MOGASA amesemakuwa wamefanikiwa kuokoa fedha hizo katika kipindi cha julai 2017 mpaka februali 2018.
MOGASA ameasema kuwa licha ya kuwepo kesi mahakamani lakini kuna kesi zingine wanashindwa na zingine wanashinda kutokana mashahidi kuosekana mahakamani inapelekea takukuru kushindwa kesi
AIDHA mkurungezi wa takukuru MOGASA MOGASA  amewataka wananchi kushirikiana na takukuru kwa uaminifu na wala wasiogope kutoa tarifa wanapoona sehem frani kuna rushwa inatokea kwani takuru ipo kwajili ya watu wote
Uwepo wa taarifa za maandishi au za mdomo kuhusu kugawanya mirathi pale mwenye mali anapofariki dunia huondoa migogoro katika familia na jamii kwa jumla.
Akizungumza Wakili wa Kujitegemea katika Ofisi ya Wakili MTAKI,Wakili TERESIA FABIAN amesema wosia unapoachwa na marehemu unapunguza migogoro inayoweza kujitokeza katika familia.
Naye Mwanamke aliyedhulumiwa mali na ndugu wa marehemu mume wake katika kijiji cha IGALULA wilayani UYUI,MWAJUMA ALI amesema baada ya mume wake kufariki dunia bila kuacha wosia ndugu wa marehemu walichukua mali zote na kumwacha na watoto wanne bila msaada wowote.
Kwa upande wake,Mwanasheria kutoka Kituo cha Msaada wa Kisheria na Haki za Binadamu,YUSUPH SALMIN anaeleza ni kwa jinsi gani wanawasaidia wahanga wanaodhulumiwa mirathi.
Afisa Maendeleo ya Jamii wa Halmashauri ya Manispaa ya TABORA,ENEMBORA LEMA amesema wao kama serikali wanatoa elimu na kuwaelekeza namna ya kupata msaada wa kisheria wahanga wa mirathi.
Ameongeza kuwa wananchi wanapoandika mirathi wanapata uhakika wa kuacha mali au vitu vyao katika sehemu salama.
………….
KIMATAIFA
Maafisa wa Mamlaka ya Taifa ya Usalama Barabarani (NTSA) pamoja na Shirika la Msalaba Mwekundu Kenya wametoa ushauri ambao unaweza kukufaa sana wakati huu wa mvua.

1.   Fahamu kwamba wakati wa kiangazi, vumbi, mchanga na taka za aina mbalimbali hurundikana barabarani. Mvua inaponyesha, husababisha barabara kuwa telezi na kwa hivyo ukiwa na gari ni muhimu kutoendesha gari lako kwa mwendo wa kasi kupindukia kwani gari likiteleza utashindwa kulidhibiti gari lako kwa urahisi.
2.   Kwa sababu ya maji, huwa vigumu sana kupiga breki wakati wa mvua na hivyo hatari ya mwenye gari kumgonga anayetembea barabarani huwa juu. Unashauriwa kutoendesha gari kwa mwendo wa kasi.
3.   Kwa sababu ya mvua, wapita njia mara nyingi hutembea wakiwa wameinamisha vichwa chini na huenda wasilione gari linapokaribia. Wenye magari wanashauriwa kuwa makini zaidi wanapofika kwenye vivuko barabarani au wanapomuona mtu akivuka barabara. Kwa wanaotembea kwa miguu, wanashauriwa kutumia vivuko vilivyotengwa na kuchukua tahadhari zaidi pia.
4.   Kwa wenye magari, iwapo barabara imefurika maji, ni vyema kutafuta barabara nyingine ya kupitia badala ya kujaribu kupitia ndani ya maji. Huwa vigumu kukadiria kina cha maji barabara inapofurika.
5.   Wakati mvua inaponyesha, wenye magari wanatakiwa kuwasha taa kuwawezesha kuona mbele na pia kutokaribia sana magari yaliyo mbele yao. Maji yanayorushwa na gari lililo mbele yanaweza kutatiza mwenye gari iwapo atakuwa karibu sana. Ushauriwa kufuata kanuni ya sekunde 3, hicho ndicho kipindi kinachochukuliwa na binadamu kuona jambo na kuchukua hatua. Usipofanya hivi, kufikia wakati unapoona aliye mbele yako amesimama na kuchukua hatua utakuwa tayari umesababisha ajali.
6.   Breki za gari huathiriwa na maji, kwa hivyo unapoendesha gari eneo lenye maji, ni vyema kuendesha gari kwa mwendo wa polepole. Hii itaziwezesha breki kukauka.
7.   Madereva wanashauriwa pia kutumia mikono yao miwili kudhibiti mwelekeo wa gari kuhakikisha wanadhibiti vyema gari.
8.   Wapita njia, waendesha baiskeli na waendeshaji pikipiki wanashauriwa kuvalia mavazi yanayoweza kuonekana vyema au mavazi yanayoweza kuakisi mwanga. Haya yatamuwezesha mtu kuonekana na madereva na kumpungushia mtu hatari ya kugongwa.
9.   Usiendeshe gari lako ndani ya maji yanayosonga, yawe kwenye mifereji au kwenye mto. Huwa vigumu sana kukadiria nguvu ya maji. Magari mengi husombwa na maji madereva wakijaribu kuvuka mito au wakitumia madaraja yaliyofurika maji. Mvua pia hudhoofisha madaraja, jambo ambalo huenda usifahamu. Daraja linaweza kubomolewa bila ufahamu wake wewe nawe ukaingia mtoni ukitarajia daraja bado lipo. Maji ya kina ya futi moja yanaweza kusomba gari lako. Kwa binadamu anayetembea, inchi sita za maji zinaweza kukusomba.

10.                   Ukiwa na gari lako, hakikisha vipangusia kioo vya gari lako  vinafanya kazi. Hili litakuwezesha kupangusa kioo na kuona mbele unapokuwa barabarani.
11.                   Iwapo una gari na limeanza kuteleza, achilia mafuta na kulielekeza gari upande ambao unateleza. Ukianfanikiwa kudhibiti gari, anza kulainisha magurudumu tena na kurejea barabarani. Hakikisha kwamba unabaki kuwa tulivu na usichukue hatua yoyote ghafla.
12.                   Usiende kwa mwendo wa kasi. Iwapo una safari ya mbali, anza mapema kuhakikisha kwamba haukumbwi na shinikizo la kutaka kwenda kwa kasi ndipo ufike.
13.                   Unapokuwa unaendesha gari, usishawishike kutumia simu yako au kufanya jambo lolote ambalo litakuzuia kuwa makini ukiliendesha gari.
14.                   Iwapo utakuwa safarini, usiegeshe gari lako au kuanza kufanya shughuli zako karibu na mto wakati wa mvua.
15.                   Ni vyema kusikiliza vituo vya redio na runinga kujifahamisha kuhusu yanayojiri na ni wapi mvua kubwaimenyesha au mafuriko kutokea.
16.                   Usitembee kwenye maji au maeneo yenye matope ambayo kuna uwezekano kwamba kuna nyaya za umeme ambazo zimeanguka. Nyumba yako ikifurika maji pia, hakikisha umezima stima.
17.                   Iwapo unatembea kwa miguu, tumia fimbo au kijiti kukadiria kina cha maji.

18.                   Mafuriko yakitokea eneo ulipo, mara moja kimbilia maeneo yaliyo juu na salama.



No comments