Header Ads

Waandamanaji saba wa Kipalestina wameuwawa kwa kupigwa risasi na askari wa Israel

Image result for Waandamanaji saba wa Kipalestina

Waandamanaji saba wa Kipalestina wameuwawa kwa kupigwa risasi na askari wa Israel na wengine zaidi ya 450 wamejeruhiwa wakati wa maandamano yaliyofanyika karibu na mpaka kati ya Gaza na Israel, kulingana na msemaji wa Wizara ya Afya ya Gaza, Ashraf al-Qedra.

 Mpalestina mmoja aliuwawa baada ya kupigwa risasi ya tumbo huko mashariki mwa Jabalia katika eneo la kaskazini mwa Ukanda wa Gaza, na vijana wengine wawili waliuwawa baada ya kupigwa risasi kichwani huko mashariki mwa mji wa Rafah kusini mwa Ukanda wa Gaza.

 Msemaji huyo wa wizara ya afya amesema machafuko yalianza leo asubuhi wakati askari wa Israel waliokuwepo kwenye mpaka kufyatua gesi ya machozi ili kuwatawanya mamia ya Wapalestina waliokuwa wanaelekea kwenye uzio wa mpaka. Kulingana na mashahidi,

 waandamanaji hao waliwarushia askari mawe. Chama cha Hamas kinacho tawala kwenye Ukanda wa Gaza kimeandaa maandamano hayo ili kusisitiza haki ya wakimbizi wa Kipalestina na vizazi vyao ya kurejea Palestina.

No comments