Header Ads

BABA AMZIKA MTOTO WAKE


Image result for Amzika mtoto wake akiwa hai




Polisi wa Migori nchini Kenya wanachunguza kifo cha mtoto mwenye umri wa miezi 
6, ambaye inasemekeana alifukiwa akiwa hai na baba yake mzazi.

Kwa mujibu wa kiongozi wa eneo hilo Chief Fredrick Owino, mwanaume huyo
 aliyetambulika 
kwa jina la Marcellus Odek, alirudi nyumbani kwake akiwa amelewa na kuchukua
 jembe

na kuchimba kaburi, ambalo alimzika mtoto huyo ambaye ameelezwa alikuwa 
akisumbuliwa
 na tatizo la kupumua.
Taarifa zaidi zinasema kwamba mama wa mtoto huyo Annah Auma wakati tukio 
linatokea alikuwa amepoteza fahamu kutokana na tatizo la kifafa alilokuwa nalo, na 
alifanya tukio hilo mbele ya familia yake na majirani, usiku wa Machi 14 mwaka huu.
Ndugu wa familia hiyo Milicent Achieng amesema mtuhumiwa aliwakuta nyumbani 
na moto akiwa anapumua, kabla hjaanza kuchimba kaburi na kumfukia, na alipoomba 
msaada kwa watu walikataa nakumshauri akimbie kwani huenda angemuua na yeye.

No comments