Header Ads

Serikali yakiri suala la umri


Image result for Dkt. Avemaria Semakafu

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dkt. Avemaria Semakafu amefunguka na kuweka wazi utata ulioibuka kuhusu kigezo cha umri wa kujiunga na masomo ya kidato cha tano na sita na kusema taarifa ambayo inasambaa imekuwa na makosa.

Semakafu amesema hayo alipoongea na www.eatv.tv na kusema kuwa yametokea makosa ya kiuandishi ila kujiunga na masomo ya kidato cha tano na sita ni miaka 25 na siyo miaka 20 kama ambavyo inasomekana katika taarifa aliyotolewa mapema leo. 
"Kumetokea makosa ya kiandishi, miaka ni 25 ya kujiunga sekondari na sio 20 kama ambavyo inasomeka kwenye ile karatasi"  alisema Semakafu 

No comments