Header Ads

Baraza la vijana wa chama cha Demokrasia na maendeleo Chadema la toa msaada wa chakula



Image result for picha KITUO CHA BUHANGIJA




Baraza la vijana wa chama cha Demokrasia na maendeleo Chadema-BAVICHA tawi la mulepa kata ya ndala Katika manispaa ya Shinyanga limetoa msaada wa vyakula na mavazi kwa watoto wenye ulemavu wanaolelewa katika kituo cha BuhangijaJumuishi,ilikupunguza changamoto zinazowakabili.


Msaada uoliotolewa na baraza hilo la vijana wa chama cha Demokrasia na Maendeleo chadema,ni Pamoja na  mchele,mafuta ya kupikia sabuni,vifaa vya kufanyia usafi,nguo na viatu vyote vikiwa na thamani ya shilingi Laki mbili
Akizungumza mara baada ya kukabidhi msaada huo kwa mlezi wa kituo hicho,mwenyekiti wa BAVICHA tawi la Mlepa kata ya Ndala bwana AFRED MASANJA amesema vijana hao wameguswa na kuona umuhimu wa kusaidia kituo hicho ambacho kina upungufu wamahitaji.

                               
Mmoja wa wajumbe wa serikali ya mtaa wa Mulepa, bwana JOHN ROBERT  ameahidi kuendelea kusaidia na kushirikiana na kituo hicho kwa hali na mali ili kusababisha chakula hakikose kani shuleni hapo
                                    
Kwa upande wake mlezi wa kituo hicho  bwana STANLEY WAGALA amewashukuru baraza la vijana wa chama cha Demokrasia na maendeleo akisema waendelee kujitolea ili kusaidia watotohao.
                                  


KITUO CHA BUHANGIJA Jumuishi kilichopo katika manispaa ya Shinyanga kinalea watoto wenye ulemavu mbali mbali wakiwemo wenye albinism,wasioona,na viziwi.

No comments