Header Ads

MSAADA UMETOLEWA KWA WAZEE NA VIJANA WASIOJIWEZA KOLANDOTO MKOANI SHINYANGA


Image result for picha ya  TAKUKULU




Jamii imeombwa kuwa na moyo wa kuwasaidia wazee wasiojiweza wanaoishi katika kituo cha KOLANDOTO kilichopo katika manispaa ya Shinyanga ambao wanakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo upungufu wa mahitaji muhimu.

Akikabidhi msaada wa vitu mbalimbali kituoni hapo, mkuu wa taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa TAKUKURU katika mkoa wa Shinyanga Bw. AMOSI GASTO MKONO amewaomba wananchi wa Shinyanga kuendelea kuwasaidia wazee hao ambao wanakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo upungufu wa chakula na uchakavu wa majengo wanayoishi.

Mkuu huyo wa TAKUKURU pia ameahidi kumsomesha mtoto mmoja miongoni mwa watoto wanne waliofaulu kujiunga na kidato cha kwanza mwaka kesho 2017,ambao wazazi wao walikuwa wanaishi katika kituo hicho na baadaye kufariki dunia.

Naye afisa mfawidhi wa kituo hicho Bi. SOFIA KANG’OMBE amesema licha ya kituo hicho kukabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo upungufu mkubwa wa chakula na mavazi ,majengo wanayoishi wazee hao ambayo  yalijengwa tangu mwaka 1984 mpaka sasa bado hayajakarabatiwa hali iliyosababisha yawe na nyufa na kutishia usalama wa wazee hao.


Badhi ya misaada ambavyo imetolewa na TAKUKURU mkoa wa Shinyanga katika kituo hicho ni pamoja na vyakula,nguo na sabuni ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya kilele cha siku ya maadili nchini Tanzania.


ANGALIA VIDEO YA MAAZIMISHO 55 YA UHURU


No comments