Header Ads

WATAO HUJUM TASAF KUCHUKULIWA HATUA


Image result for picha ya TASAF






Walengwa wa TASAF awamu ya tatu Mpango wa kunusuru kaya masikini mkoa wa Shinyanga wameombwa kutoa taarifa dhidi ya watendaji watakaohusika kufanya hujuma hasa vitendo vya rushwa,katika utekelezaji wa mpango huo

Mratibu wa TASAF Mkoa wa Shinyanga bwana Dotto Maligisa amewaomba walengwa kutoa taarifa Pale watakapobaini kuwepo udanganyifu wowote utakaofanywa na watendaji zikiwemo kamati za usimamizi ngazi ya serikari ya mtaa,kitongoji na kijiji,ikiwemo mianya ya rushwa.
                               

Hatua hiyo ni kufuatia tetesi kutoka kwa baadhi ya wananchi kwamba baadhi ya watendaji hutumia fursa hiyo kuwashawishi walengwa kugawana nao Pesa wanazopokea kwenye mpango huo.
Mratibu huyo wa TASAF Mkoa wa Shinyanga amesema tayari Mkoa wa Shinyanga umefanikiwa kuwafikia walengwa 34,883 kati ya 45,000 waliokuwa wametarajiwa.
Aidha amesema kati ya walengwa hao 641 wameondolewa kwenye mpango kutokana na kukosa sifa.
                     

Asema TASAF awamu ya tatu mpango wa kunusuru kaya masikini umeleta matokeo cmehanya baada ya walengwa wengi kujikwamua kiuchumi katika maeneo ya kilimo,ufugaji na ujenzi


No comments