Header Ads

chadema mkoani tabora kuwasimamisha kazi


Image result for chadema


Chama cha demokrasia na maendeleo CHADEMA mkoani TABORA kimewasimamisha kazi kwa muda usiojulikana viongozi wake wawili wa ngazi ya wilaya ambao ni mwenyekiti wa wilaya ya Igunga  JOSEPH KASHINDYE na katibu wake IDDY ATHUMANI .

Katibu wa chadema mkoa wa Tabora  ALLY MWAKILIMA amesema viongozi hao wamesimamishwa uongozi tangu tarehe 30 mwezi uliopita baada ya kukiuka katiba  ya chama hicho. 

Viongozi waliosimamishwa ni mwenyekiti JOSEPH KASHINDYE na katibu wake IDDY ATHUMANI wamekiri kupokea barua ya kusimamishwa uongozi tangu tarehe 3 mwezi huu ameeleza kuwa maamuzi  ya kuwasimamisha yametolewa  na baraza la uongozi la Mkoa kupitia  chama hicho baada ya viongozi hao wawili kudaiwa kukiuka na kuvunja katiba  ya chama

Mwezi ulipita viongozi hao wawili walisimama mbele ya mahakama  ya wilaya iliopo mkoani TABORA kutoa ushaahidi  kwa upande wa mtu alieshitaki chama huku  huku wakiwa wanajua wazi kuwa nikinume na katiba ya chama hicho.


Amebainisha kuwa pamoja na  kuwasimamisha viongozi hao pia baraza la chama limemuagiza katibu wa wa chama hicho IDDY ATHUMANI kukabidhi mali zote za chama kwa katibu wa jimbo la Igunga mbele ya mwenyekiti wake ikiwa ni pamoja na kujieleza ndani ya siku nne

No comments