Header Ads

mwanafunzi wa kike kutozwa 200,000


Image result for picha ya hela ya kitanzania
 MKUU wa Mkoa wa Singida, Mathew Mtigumwe ameagiza kukamatwa na kufunguliwa mashitaka Mwenyekiti wa Baraza la usuluhishi Kata ya Rungwa wilayani Manyoni, kwa tuhuma za kumtoza faini ya Sh 200,000 mwanafunzi wa kike anayedaiwa kujihusisha na vitendo vya ngono.

Mwenyekiti huyo, Zuberi Manjemi anadaiwa kumtoza faini hiyo mwanafunzi wa darasa la nne kisha kumwachia bila adhabu yoyote kijana aliyedhaniwa kuwa ni mpenzi wa binti huyo, hali iliyozua hasira ya wazazi wa binti huyo na kuamua kutoa malalamiko yao kwenye mkutano wa hadhara.

Katika utetezi wake, Mwenyekiti huyo alidai kuwa aliamua kumtoza faini binti huyo pekee baada ya kukiri kupokea simu ya mkononi kutoka kwa mvulana huyo, hivyo alitoa adhabu hiyo ili iwe fundisho kwa wananfunzi wengine wa kike.

Utetezi huo ulitupiliwa mbali na Mkuu wa Mkoa na kuagiza mwenyekiti huyo akamatwe kwa kosa la kutoa adhabu ya upande mmoja huku akimwachia huru mtuhumiwa wa kiume aliyemrubuni mwanafunzi huyo kufanya naye mapenzi.

Habari zilizopatikana eneo la tukio zinadai kuwa baada ya walimu wa shule ya Msingi Rungwa, kutilia shaka umiliki wa simu ya mkononi ya mwanafunzi huyo, walimhoji na alikiri mwenyewe kupewa na mvulana huyo.

Walimu hao walidai kuweka mtego kwa mwanafunzi huyo kumpigia mvulana huyo na kutokana na mazungumzo yao walibaini kuwa wana mahusiano ya kimapenzi ya muda mrefu, hivyo kuamua kuwapeleka baraza la kata ambapo mwanafunzi alitozwa faini na mpenzi wake kuachiwa huru.

No comments