Header Ads

Waziri wa ardhi,nyumba na maendeleo ya makazi WILLIAM LUKUVI ameitaka idara ya ardhi katika mkoa wa Shiyanga kutoa hati






Waziri wa ardhi,nyumba na maendeleo ya makazi WILLIAM LUKUVI  ameitaka idara ya ardhi katika mkoa wa Shiyanga kutoa hati ya umiliki wa viwanja  kwa wananchi ili kuiwezesha serikali kupata mapato.

Akizungumza na watumishi wa idara hiyo katika kikao maalum kilichofanyika leo kwenye  ukumbi wa mkuu wa mkoa wa Shinyanga LUKUVI amesema takwimu zinauonyesha mkoa wa Shinyanga kuwa una idadi kubwa ya watu wenye viwanja vilivyopimwa lakini hawana hati za umiliki wa viwanja.

Amesema mpaka sasa mkoa wa Shinyanga una idadi ya watu 1200 tu ambao wana hati miliki za viwanja vyao jambo ambalo licha ya kuikosesha mapato serikali ambayo lingeyapata kupitia kodi za majengo hali hiyo pia inawafanya wananchi wengi wakose mikopo kutoka taasisi mbalimbali za kifedha.

WAZIRI LUKUVI pia amewapiga marufuku maafisa wa ardhi kuchukua viwanja au mashamba ya wananchi bila kuwalipa fidia inayoendana na thamani halisi ya ya ardhi zao  huku akiwataka maafisa wanaohusika na mipango miji kuhakikisha wanaweka mikakati ya kupanga mji kikamilifu  ili kuepuka ujezi holelela.




Walengwa wa TASAF awamu ya tatu Mpango wa kunusuru kaya masikini mkoa wa Shinyanga wameombwa kutoa taarifa dhidi ya watendaji watakaohusika kufanya hujuma hasa vitendo vya rushwa,katika utekelezaji wa mpango huo
Mratibu wa TASAF Mkoa wa Shinyanga bwana Dotto Maligisa amewaomba walengwa kutoa taarifa Pale watakapobaini kuwepo udanganyifu wowote utakaofanywa na watendaji zikiwemo kamati za usimamizi ngazi ya serikari ya mtaa,kitongoji na kijiji,ikiwemo mianya ya rushwa.
                              
Hatua hiyo ni kufuatia tetesi kutoka kwa baadhi ya wananchi kwamba baadhi ya watendaji hutumia fursa hiyo kuwashawishi walengwa kugawana nao Pesa wanazopokea kwenye mpango huo.
Mratibu huyo wa TASAF Mkoa wa Shinyanga amesema tayari Mkoa wa Shinyanga umefanikiwa kuwafikia walengwa 34,883 kati ya 45,000 waliokuwa wametarajiwa.
Aidha amesema kati ya walengwa hao 641 wameondolewa kwenye mpango kutokana na kukosa sifa.
                               

Amesema TASAF awamu ya tatu mpango wa kunusuru kaya masikini umeleta matokeo chanya baada ya walengwa wengi kujikwamua kiuchumi katika maeneo ya kilimo,ufugaji na ujenzi


No comments