Header Ads

Serikali ya wilaya ya shinyanga imeahidi kutatua mgogoro wa ardhi

Image result for picha ya ardhi


Serikali ya wilaya ya shinyanga imeahidi kufuatilia na kuhakikisha inatatua mgogoro wa ardhi uliopo katika mtaa wa Luhende kata ya Ndala  katika Manispaa ya Shinyanga.

Akizungumza na wakazi wa mtaa wa Luhende katika kata ya Masekelo kwenye mkutano maalumu uliokuwa na lengo la kusikiliza kero za wananchi hao kuhusu mgogoro wa ardhi,mwakilishi wa ofisi ya mkuu wa Wilaya ya Shinyanga,CHARLES MAUGILA amewaomba wananchi hao kuwa wavumilivu wenye subira ili kutoa nafasi kwa watendaji kufuatilia ili kupata ufumbuzi.

Bwana MAUGILA amesema kuwa viashiria vyovyote vya migogoro si ishara njema katika ustawi wa maendeleo ya Jamii kwani inaweza kuwa chanzo cha uvunjifu wa Amani.Awali wakazi wa mtaa wa Luhende kata ya Masekelo katika mkutano maalumu na maafisa kutoka ofisi ya Mkuu wa wilaya na wale wa ardhi manispaa,wamelalamikia

 kero ya mgogoro wa ardhi ambao wamesema umesababishwa na maafisa wa ardhi kukosa uaminifu na kushindwa kutekeleza majukumu yao kwa uadilifu
Wananchi hao wameiomba ofisi ya mkuu wa wilaya kwa kushirikiana na ofisi ya ardhi katika Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga kushughulikia na kutatua kero zilizopo ili kumaliza migogoro ya ardhi.

                                                     ---

Kwa upande wake afisa ardhi wa Manispaa ya Shinyanga bwana ALEX  RUTAHILWA amewaomba wananchi wote wenye migogoro ya ardhi kuhakikisha wanazingatia taratibu zote zilizopo kisheria,ambapo pia ameshauri  masuala  yote yaliyopo mahakamani yasijadiliwe kwa kuwa kila ngazi inafanya kazi kwa mujibu wa miongozo. 

No comments