Header Ads

Waandishi wa Habari Mkoani Shinyanga kuielimisha jamii



Image result for picha ya waandishi shinyanga
copy kwanye google 

Waandishi wa Habari Mkoani Shinyanga wamesema  wataendelea kuielimisha Jamii Juu ya Dhana ya watu wenye ualbino ili Jamii iweze kufahamu na kuelewa kuwa kundi hilo lina haki sawa na watu wengine.

Wameyasema hayo leo wakati wakijadiliana kwenye warsha ya siku moja iliyofanyika kwenye hotel ya Empire iliyopo mjini Shinyanga,kwamba ni wajibu wa vyombo vya habari kuendelea  kuifahamisha Jamii Juu ya Madhara ya kuwaua albino, kwani kuwaua ni ukiukaji wa haki za binaadamu.


 Afisa mahusiano wa habari  wa chama cha watu wenye ualbino Tanzania JOSEPHAT TONA amesema  Warsha hiyo ya siku moja imeandaliwa na chama cha watu wenye ualbino ngazi ya Taifa kwa ufadhiri wa shirika la Open society foundations ikilenga kukutana na waandishi wa habari ili kubadilishana mawazo,kujadili na kuona changamoto wanazokabiliana nazo watu wenye ualbino na kisha kuona namna ya kuzitatua.

No comments