Header Ads

JESHI la Polisi Kanda Maalumu ya Tarime /Rorya linawashikilia watu wawili ambao ni ngariba

Image result for PICHA YA JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Tarime

JESHI la Polisi Kanda Maalumu ya Tarime /Rorya linawashikilia watu wawili ambao ni ngariba kwa tuhuma za kuwakeketa wanafunzi wawili wanaosoma darasa la tatu katika Shule ya Msingi Nyankoni na kuwasababishia majeraha na maumivu makali.

Ngariba hao ni Angelina Kirimi (50) na Mwita Ryoba (54), wote wakazi wa kijiji cha Itiryo, tarafa ya Ingwe, wilayani Tarime.

Kamanda wa Polisi Tarime Rorya, Andrew Satta alisema kuwa ngariba hao walifanya vitendo hivyo vya kikatili vya kuwakeketa wanafunzi wawili wa kike ambao majina yao yamehifadhiwa kati ya Desemba 5 na 7 mwaka huu.

Alisema Jeshi la Polisi kwa kushirikiana na mashirika ya kupinga ukatili na unyanyasaji kwa mtoto wa kike likiwemo la ATFGM la Kanisa Katoliki Masanga, waliweza kuwabaini wanafunzi hao kukeketwa baada ya wanafunzi hao kufanyiwa uchunguzi na Dawati la Jinsia na madaktari.

Kamanda alisema , “Watuhumiwa hao ambao ni ngariba tunawashikilia kwa mahojiano zaidi na kisha tutawafikisha mahakamani kujibu tuhuma za kudhuru mwili.


 Jeshi letu linawaonya kwa wale wote wakaokamatwa wakiwashawishi watoto wa kike kwenda kukeketwa wakiwemo wazazi, wanaowapeleka kuwasindikisha watoto wa kike kwenda kukeketwa na wakeketaji wenyewe ambao ni mangariba kama hawa tuliowakamata”.

Alisema ukeketaji unaofanywa kwa watoto wa kike umepigwa marufuku kwani ni moja ya ukatili na unyanyasaji wa kijinsia.

Kamanda alisema wana taarifa za kitabibu kuwa wasichana waliokeketwa hupata matatizo ya kutokwa damu nyingi wakati wa kujifungua na kusababisha vifo na jamii inatakiwa kuacha mila zilizopitwa na wakati ambazo zina madahara kwa jamii zikiwemo hizo za ukeketaji.


angalia video mpya ya vanesa mde na mmewe juma jux



No comments