Header Ads

UCHUMI UMEKUWA MGUM MKOANI SHINYANGA




Image result for PICHA YA MAHINDI KUNYAUKA SHAMBANI



Kutokana na mvua kuchelewa kunyesha kwa wakati katika  Mkoani SHINYANGA imepelekea hali ya kiuchumi kuwa ngumu katika msimu huu wa sikukuu za mwishoni mwa mwaka hali inayopelekea wananchi kutopata mazao ya chakula kwa wakati

Wakizungumza na Redio Faraja FM kwa nyakati tofauti Baadhi ya wananchi wametoa maoni yao juu ya hali ya kiuchumi katika msimu huu wa sikukuu za mwishoni  mwa mwaka na msimu wa sikukuu za mwishoni mwa mwaka uliopita nakusema kuwa mazao ya chakula  ndiyo wanayotegemea sana katika misimu yote ya sikukuu za mwishoni mwa mwaka

Aidha wamesema sababu nyingine kubwa ambayo imesababisha ugumu wa kiuchumi katika msimu huu wa sikukuu ni mfumko wa bei ambao pia unasababishwa na ulipaji wa ushuru kwa wafanyabiashara wakati biashara wanazofanya kuwa ngumu kutokana na wateja kukosa mazao ya chakula ambayo ndiyo yanategemewa katika hali ya kiuchumi

pia wamesema kutokana na mfumko huo wa bei umesababisha bidhaa nyingi kuadimika katika soko kuu la mjini shinyanga na kupelekea watu wengi kubadilisha sehemu ya kufanyia mahemezi na kuelekea  katika soko la NGUZO NANE ambako wanaamini kunaupungufu wa bei ya bidhaa hizo


hatahivyo wameiomba serikali kutoa punguzo la ushuru kwa wafanyabiashara ilikuweza kushuka kwa bei ya bidhaa hizo na kuwafanya wananchi kunufaika na huduma ya bidhaa zilizopo katika soko kuu  mjini humo kwa kipindi hiki cha sikukuu za mwishoni mwa mwaka

No comments