Header Ads

Mtu mmoja mtembea kwa miguu amefariki papo hapo baada ya kugongwa na gari






ACP MULIRO JUMANNE MULIRO



Mtu mmoja mtembea kwa miguu amefariki papo hapo baada ya kugongwa na gari na wengine wawili kujeruhiwa katika ajali ya  barabarani  iliyotokea jana majira ya saa mbili na nusu usiku katika eneo la buhangija kona kata ya ibinzmata  katika manispaa ya shinyanga

Akitoa taarifa ya ajali hiyo kamanda wa jeshi la polisi mkoa wa shinyanga MULIRO  JUMANNE MULIRO amemtaja aliyepoteza maisha kuwa ni KHADIJA PHILIPOmwenye umri wa miaka  25, mkazi wa ndembezi ambaye alikuwa akitembea kwa miguu,na waliojeruhiwa ni  CHRISTINA SULEIMAN miaka 40, mkazi wa Nindo mtembea kwa miguu,Pamoja  na AGNESS NDAMA mwenye umri wa miaka  25, mkazi wa Mwanza ambaye alikuwa abiria katika gari hilo.

Kamanda murilo amesema katika uchunguzi wa awali jeshi la polisi limebaini kuwa chanzo cha ajali hiyo ni uzembe wa dereva wa gari hilo lenye namba za usajili T 247 ACX TOYOTA LAND-Cruza
                                                  
Kwa upande wa mashuhuda a ajali hiyo wamesema kuwa mwendo kasi wa dereva katika eneo la kona na ukosefu wa baadhi ya alama muhimu za barabarani umechangia kwa kiasi kikubwa kutokea kwa ajali hiyo
                         
Aidha kamanda MULIRO amesema jitihada za kumpata dereva ambaye ndio kiini cha ajali hiyo zinaendelea huku akitoa  wito kwa madereva kuzingatia kanuni na taratibu za barabari ili kuepusha ajali zinazoweza kuepukika 



No comments