Header Ads

Ligi kuu nchini Uingereza imeendelea tena leo hii kwa michezo mbalimbali kupigwa katika viwanja tofauti.

Ligi kuu nchini Uingereza imeendelea tena leo hii kwa michezo mbalimbali kupigwa katika viwanja tofauti.




Huko Wembley kikosi cha Tottenham kimefanikiwa kuchomoza na ushindi wa mabao 2 – 0 dhidi ya Huddersfield Town na hivyo kuwasogelea kwa ukaribu Manchester United inayoshika nafasi ya pili.
Mabao ya Spurs yakifungwa na kiungo wao raia wa Korea Kusini, Son Heung-min dakika ya (27 na 54).
Swansea nao wakiwa katika dimba la Liberty wamefanikiwa kuchomoza na ushindi mnono wa mabao 4 – 1 dhidi ya West Ham.
Waliyokuwa mwiba mkali katika mchezo huo kwa upande wa Swansea ni Ki Sung-yueng, Van der Hoon, King na J Ayew wakati bao la West Ham likifungwa na Antonio.

No comments