Balotelli asema anajutia sana kujiunga na Liverpool
Mshambuliaji wa
Nice Mario Balotelli amesema kujiunga na Liverpool, 'ulikuwa uamuzi
mbaya zaidi aliowahi kuufanya maishani mwake.'
Mwitaliano huyo
alifunga mabao manne katika mechi 28 alizochezea Liverpool baada ya
kujiunga nao kutoka AC Milan mwaka 2014 kwa thamani ya dola milioni 16.
''Isipokuwa
mashabiki, ambao hunishabikia, na wachezaji kadhaa ambao
tunasikilizana, sipendi klabu yenyewe," Balotelli ameiambia runinga ya
Ufaransa ya Canal Plus.
Mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 26, alisema
hayo kabla ya kufunga mabao mawili katika mechi yake ya kwanza na klabu
ya Nice katika michuano ya Ligue 1 walipofunga mabao 3-2 dhidi ya
Marseille siku ya Jumapili.
Meneja Brendan Rodgers, aliyemsajili
Balotelli, alipigwa kalamu na Liverpool mwezi Oktoba mwaka 2015, na
Jurgen Klopp akachukua hatamu.
Post a Comment