Header Ads

David Nkulila amejiuzuru nafasi ya ujumbe kwenye kamati ya Fedha na utawala kwa kile alichokieleza ameshindwa kukubaliana na baadhi ya mambo yanavyoamuliwa










Diwani wa kata ya Ndembezi katika Manispaa ya Shinyanga David Nkulila amejiuzuru nafasi ya ujumbe kwenye kamati ya Fedha na utawala kwa kile alichokieleza ameshindwa kukubaliana na baadhi ya mambo yanavyoamuliwa katika kamati na baraza.


Ameyasema hayo leo  wakati akizungumza na  vyombo vya habari kwenye kikao maalumu kilichofanyika kwenye klabu ya waandishi wa habari wa mkoa wa Shinyanga mjini hapa.

Mheshimiwa Nkulila amesema hatua ya kujiuzuru kwake katika nafasi hiyo ni ishara ya kutokubaliana na na baadhi ya mambo ambayo yanakiuka sheria,kanuni na taratibu.
Ameyataja baadhi ya mambo yaliyosababisha yeye kujiuzuru katika kamati hiyo ya Fedha na utawala kuwa ni Pamoja na udanganyifu uliofanyika ambapo baraza la madiwani la manispaa ya Shinyanga liliandaa bajeti na kuiwasilisha wizarani,kutotekelezeka kwa sheria ya ujenzi wa nyumba za ghorofa kutokana na mianya ya rushwa,lakini mgogoro wa greda,hoja za barabara za lami ambapo ambapo zimekuwa zikitajwa kilometa nyingi tofauti na uhalisia.







                              Diwani nkulila amesema amefikia uamuzi wa kujiuzuru katika nafasi hiyo ya ujumbe wa kamati ya fedha na utawala, baada ya kutafakari kwa kina Juu ya utata kuhusu mambo kadhaa yanayojitokeza katika Halmashauri ya manispaa ya Shinyanga ambayo ni kinyume na matarajio lakini pia  yana athari kwa wananchi ambao walimwamini na kumpa  dhamana ya uongozi.




Mheshimiwa Nkulila akizungumza na waandishi wa habari

No comments