Header Ads

watu zaidi ya 99 wafariki kwenye ajali ya treni India

 watu  zaidi ya 99 wafariki kwenye ajali ya treni India

Waokoaji wanakata mabaki kuwafikia watu waliokwama ndani
Idadi ya watu waliyofariki kutokana na ajali ya treni iliyotokea mapema leo kaskazini mwa India, imeongezeka hadi tisini na tisa na kuwajeruhi mamia ya wengine.
Treni hiyo ilikuwa ikitoka Indore kuelekea Patna kabla ya kupoteza muelekeo na kutoka katika barabara ya reli na kuanguka ilipokaribia mji wa Mashariki wa Kanpur katika jimbo la Utter Pradesh.

Maafisa wa kutoa huduma za dharura wanajaribu kuwaokoa manusura waliokwama katika mabehewa yaliyoanguka.
Waziri wa uchukuzi wa India ameamuru kufanywa kwa uchunguzi kubaini kilichosababisha ajali hiyo.
Wengi wa waliokufa walikuwa kwenye mabehewa yaliyokuwa karibu na injini


chanzo bbc

No comments