Header Ads

Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro ameonya madiwani



Image result for picha ya mkuu wa wilaya ya shinyanga





Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro ameonya madiwani wa halmashauri ya manispaa ya Shinyanga kujitengeneza vikao kiholela ambavyo havina tija kwa madhumuni ya kujipatia Posho.

Matiro amezungumza haya leo kwenye baraza la dharula la madiwani hao lililokuwa na ajenda moja kuu ya kujadili taarifa za ubovu wa Grade lillilokuwa likituhumiwa na baadhi ya madiwani hao kuwa  haliwezi kufanya kazi ambalo limegharimu milioni 520.
Matiro amesema baada ya kusikiliza majadiliano ya Greda hilo amebaini tatizo hilo kila diwani analifahamu, ambalo lilipaswa kuisha kwenye kikao kilichopita cha Oktoba 28 na 29, lakini anasiitika kwa madiwani hao kuchezea fedha ambazo zilipaswa kuelekezwa kwenye miradi ya maendeleo ya wananchi.

Aidha kufuatia kikao kikao mkuu wa wilaya amemonya mkurugenzi wa manispaa hiyo Lewis Kalinjuna kuwa endapo akirudia kuruhusu vikao vya namna hiyo vya kujitengenezea mazingara ya posho serikali haita sita kumwajibisha.
Kwa upande wake naibu Meya wa manispaa ya Shinyanga Agnes Machiya akitoa taarifa ya juu ya Greda hilo mara baada ya madiwani kujigeuza kuwa kamati, wamekubariana Greda hilo ni zima isipokuwa walichokosea ni kumpatia mtu wa kulitumia ambaye hajalisomea.

Pia amesema kutokana na tatizo hilo hivyo wameridhia kupeleka watu wawili kwenda kulisomea Greda hilo ambalo litafanya kazi mbalimbali za halmashauri ya manispaa ikiwamo uchongaji wa barabara.


Mtambo huo wa Greda ulinunuliwa mwaka jana Marchi 20, lakini kutokana na kukaa muda mrefu kwenye ofisi za halmashauri hiyo kwa kukosa Opareta wa kulitumia na lilionekana kuwa  bovu na hivyo Madiwani kuingiwa na hofu kuwa pesa za mtambo huo zimeliwa.

No comments