Header Ads

TASAF awamu ya tatu kutumia fedha kwa malengo yaliyokusudiwa


Image result for mkuu wa mkoa wa shinyanga

MKUU WA MKOA SHINYANGA Zainabu Telack 


Mkuu wa mkoa wa Shinyanga  Zainabu Telack amewaomba walengwa wa mpango wa kunusuru kaya masikini TASAF awamu ya tatu kutumia fedha kwa malengo yaliyokusudiwa badala ya kutumia kwenye mambo ya anasa

Ameyasema hayo Jana wilayani kishapu  kwamba Pesa zinazotolewa kwa walengwa waliopo kwenye mpango huo zitumike kama ilivyokusudiwa,na hasa kuwekeza kwenye Elimu,kilimo na mambo mengine ya msingi yatakayosaidia kuwainua kiuchumi.

Mkuu huyo wa mkoa amesema Pamoja na mambo mengine ya msingi walengwa wa TASAF awamu ya tatu, mpango wa kunusuru kaya masikini,wanapaswa kuwekeza kwenye Elimu ya watoto wao ili kuwajengea msingi thabiti katika maisha yao


Kwa upande wao walengwa wa mpango wa kunusuru kaya masikini TASAF awamu ya tatu wilayani kishapu wamesema fedha wanazopatiwa kwenye mpango huo zimewanufaisha baada ya kuzielekeza katika mambo ya msingi kama vile ufugaji,kilimo , ujenzi na kusomesha watoto

                                               

No comments