Header Ads

WAHARIFU WA KAMATWA SHINYANGA


Image result for PICHA YA SHINYANGA





Jeshi la polisi mkoani Shinyanga limewakamata watuhumiwa wapatao 24  ambao wanasadikiwa kujihusisha matukio mbalimbali ya kihalifu.
Kamanda wa polisi wa mkoa wa Shinyanga MULIRO JUMANNE MULIRO amesema watuhumiwa hao wamekamatwa kwa nyakati tofauti kufuatia  misako mbalimbali iliyotokana na taarifa za kiintelejensia ambayo limeifanya kwa zaidi ya wiki moja.

Amewataja watuhumiwa waliokamatwa kuwa ni pamoja na wale wanaohusika katika vitendo vya uvunjaji,wizi na unyang’anyi,pamoja na kukutwa na pombe haramu ya Ngongo na dawa za kulevya aina ya bangi.
Kamanda MULIRO pia ametoa taarifa za kukamatwa kwa watu wawili wanaosadikiwa kuhusika katika tukio la wizi wa gari lilitokea Septemba nane mwaka huu huko wilayani MAFINGA mkoani IRINGA, ambapo dereva wa gari hilo aliporwa gari lake baada ya kuuawa na kisha mwili wake kutupwa kando ya mto RUAHA.


Amesema watuhumiwa hao wamekamatwa siku ya Novemba 14 mwaka huu  majira ya saa tano asubuhi katika eneo la BIJAMORA kata ya NYIHONGO wilayani Kahama ,wakiwa na gari hilo aina ya TOYOTA CARINA lenye namba za usajili T.531 CWA. 

No comments