Header Ads

ijiji cha NHELEGANI kata ya KIZUMBI AMANI YA TAWALA




Image result for PICHA YA SHINYANGA



                                
Wakazi wa Kijiji cha NHELEGANI kata ya KIZUMBI katika manispaa ya Shinyanga wamesema hivi sasa wanaishi kwa amani baada ya kukoma kwa matukio yaliyokuwa yakihusishwa na imani za kishirikina ambapo baadhi ya wanawake walilalamikia kuingiliwa kimwili na mtu asiyejulikana.

Wakizungumza na KALI ZOTE BLOG baadhi ya wakazi wa kijiji hicho  wamebainisha kuwa hivi sasa vitendo hivyo havitokei kama ilivyokuwa hapo awali na wameiomba serikali kuhakikisha inachukua hatua za kiusalama zaidi.

Pamoja na madai hayo ya wananchi Mwenyekiti wa kijiji hicho cha NHELEGANI Bw.SENI SHIJA amendelea kukanusha kuwepo kwa matukio hayo na baada ya kuhojiwa zaidi na waandishi wa habari alikataa kuzungumza.


Siku chache zilizopita wananchi wa vijiji vya NHELEGANI na BUGAYAMBELELE kata ya kizumbi katika manispaa ya Shinyanga walilalamikia kuibuka kwa mtu ambaye alikuwa akiingia kimazingara katika nyumba zao nyakati za usiku na kisha kuchukua vitu mbalimbali ikiwemo fedha na simu za mkonani na baadaye kuwaingilia kimwili baadhi ya wanawake.

No comments