Header Ads

LIBERATUS SANGU amewataka wanafunzi waliomaliza masomo katika Seminari ya awali ya Sayusayu kuwa mfano mzuri kwa wengine


Image result for picha ya LIBERATUS SANGU




Askofu wa Jimbo katoliki la Shinyanga mhashamu LIBERATUS SANGU amewataka wanafunzi waliomaliza masomo katika Seminari ya awali ya Sayusayu kuwa mfano mzuri kwa wengine, kutenda mema na kuonyesha upendo kwa wengine

Akizungumza katika Misa maalumu ya mahafali ya 13,ya Seminari hiyo askofu SANGU amewataka wanafunzi waliohitimu masomo ya mwaka mmoja katika Seminari hiyo kuendelea kuishi maisha ya kumfuata kristu kwa kuonesha upendo,usiokuwa na Mipaka,hata kwa wale wasiokuwa wakristu,na kuwa chimbuko la kupunguza mateso kwa wengine.

Aidha amewaomba waamini kuendelea kuwaombea waseminari hao ili wale wanaotamani wito wa upadri waweze kufikia,na kwamba anaamini miongoni mwao wapo watakaofikia daraja  takatifu la uaskofu,na wengine kuwa na nyadhifa mbalimbali katika kanisa

Jumla ya wahitimu 284 wamemaliza masomo yao ya mwaka mmoja katika Seminari ya awali ya mtakatifu Gregory mkuu iliyopo Sayusayu wilayani Maswa mkoani Simiyu,ambao wanatoka katika majimbo matano yaliyopo kanda ya ziwa,ikiwemo Jimbo la Shinyanga,Mwanza,Geita,Bunda,na Musoma.

Baada ya masomo hayo waseminari hao wataanza masomo ya kidato cha kwanza mnamo Januari mwaka kesho,katika Seminari ndogo za Shanwa,Makoko,Nyegezi,na Sengerema

No comments