Header Ads

Jumla ya wanafunzi 16,907 kati ya 25,413 wa shule za msingi katika mkoa wa Shinyanga wamechaguliwa kuendelea na masomo ya sekondari


Image result for picha ya shule



Jumla ya wanafunzi 16,907  kati ya 25,413 wa shule za msingi katika mkoa wa Shinyanga wamechaguliwa kuendelea na masomo ya sekondari kidato cha kwanza kwa mwaka 2017,ufaulu ambao ni sawa na asilimia 66.53 ya waliofanya mtihani,wa kuhitimu darasa la saba mwezi septemba mwaka huu

Akitangaza matokeo ya uteuzi  wa wanafunzi watakaojiunga na kidato cha kwanza kwa mwaka wa masomo 2017,katibu tawala mkoa wa shinyanga ALBERTH MSOVELA anesema matokeo na ufaulu huo umetokana na usimamizi,utendaji na Jitihada baina ya walimu,watendaji na wanafunzi wenyewe.

Amesema  matokeo hayo  yametoa fursa kwa mkoa  kushika nafasi ya 15 kati ya mikoa 26 iliyopo hapa nchini huku shule mbili zikiwa kwenye kumi bora baada ya kushika nafasi ya kwanza na ya pili.
                               
Image result for picha ya shule



Diwani wa kata ya kambarage katika manispaa ya Shinyanga Hassan Mwendapole,ni miongoni mwa wajumbe waliohudhuria kwenye kikao cha kutangaza uteuzi wa wanafunzi, ambaye alitaka kupata ufafanuzi wa mambo kadhaa ikiwemo mgawanyo wa nafasi za kwenda kusoma shule za bweni
                             ---
Akijibu hoja ya mheshimiwa MWENDAPOLE afisa Elimu wa mkoa wa Shinyanga Mohamed Kahundi amesema ushirikiano wa wazazi kufuatilia mwenendo wa watoto,inahitaji kipaumbele na kwamba suala la kukariri lina taratibu zake kwa kuwa lipo kisera.

 Aidha  wadau wote wa Elimu waliokuwa kwenye kikao hicho  wamesisitizwa kutumia nafazi zao kuielimisha Jamii Juu ya umuhimu wa kupeleka watoto shuleni,kwani elimu ni kito cha thamani,na daraja thabiti la kumvusha mwanadamu kutoka hatua moja ya chini kwenda hatua nyingine ya mafanikio.

No comments