Header Ads

Hali ya ubinafsi na kujali maslahi zaidi

Hali ya ubinafsi na kujali maslahi zaidi imelezwa kuwa inachangia kwa kiasi kikubwa kuendelea kwa vita na mafarakano katika maeneo mbalimbali duniani.

Akizungumza katika misa ya kilele cha jubilee ya mwaka wa huruma ya Mungu, askofu wa jimbo katoliki la Shinyanga mhashamu LIBERATUS SANGU amesema binadamu wameshindwa kuwa chimbuko la amani kwa sababu ya kutawaliwa na hali ya maslahi binafsi,uchu wa madaraka na ubinafsi

Akielezea zaidi amebainisha kuwa, baada ya Mungu kumuumba binadamu alimwagiza kwenda kuvitawala vitu vyote na kuvitiisha lakini ameshindwa kufanya hivyo na badala yake kujikuta yeye mwenyewe akitawaliwa na kutishwa na vitu vya dunia kwa kuendekeza tamaa za mali,madaraka na ubinafsi mambo ambayo yamesababisha kuendelea kwa vita na mafarakano katika jamii.

Amewataka wakristu kuungana kumwomba KRISTU autawale ulimwengu ili hali ya upendo na amani iweze kurejea kwa vile binadamu wameshindwa kuwa chimbuko la amani na utulivu.

Leo askofu SANGU ameongoza misa takatifu ya kufunga jubilei ya mwaka wa huruma ya Mungu katika kanisa kuu la mama mwenye huruma la Ngokolo mjini Shinyanga, misa ambayo imekwenda sanjari na maadhimisho ya sikukuu ya KRISTU MFALME pamoja na zoezi la uwasilishaji wa zaka kiparokia.

No comments