Header Ads

MADEREVA WAOMBWA KUWA MAKINI BARABARANI ILI MKUPUNGUZA AJARI BARABARANI


Image result for picha za bodaboda





Serikali imeombwa  kuchukua hatua za kisheria dhidi ya madereva wanaotumia vilevi wakati wanapoendesha   kwani  wamekuwa wakisababisha ajali za mara kwa mara,


zinazopelekea vifo na majeruhi  hali ambayo inapunguza nguvu kazi ya Taifa.
Wakizungumza na redio faraja kwa nyakati tofauti baadhi ya wakazi wa mji wa Shinyanga wamesema kuwa licha ya kuwepo  sababu mbalimbali zinazopelekea ajali  za barabarani  lakini matumizi ya vilevi hasa Pombe kwa baadhi ya madereva ni  chanzo kikubwa

Wamezitaja sababu nyingine kuwa ni madereva kutozingatia sheria za usalama barabarani,baadhi ya abiria wasiokuwa makini  kuwashinikiza madereva waendeshe mwendo kasi,lakini pia baadhi ya askari wa usalama barabarani kushindwa kuwajibika.
                                             -

Baadhi ya madereva wametaja  baadhi ya mambo yanayochangia kutokea ajali  kuwa ni  baadhi ya askari wa  usalama barabarani kuwa wasumbufu na  kutokuwa waaminifu hali inayowavuruga kisaikolojia.
                                                   
Kwa upande wake mkuu wa Polisi kikosi cha usalama barabarani Mkoa wa Shinyanga mrakibu wa Polisi ANTONY MASANZU amesema Jeshi la Polisi lina wajibu mkubwa wa kuhakikisha linasimamia sheria ya usalama barabarani ili kudhibiti ajali.
                                            
UZEMBE KWA BAADHI YA MADEREVA KUSHINDWA KUZINGATIA SHERIA, KANUNI, NA TARATIBU ZA USALAMA BARABARANI IMEELEZWA KUWA NI CHANZO CHA KUTOKEA AJALI ZA MARA KWA MARA.



No comments