atanzania wameaswa kuitunza na kuidumisha amani iliyopo kwani ndiyo msingi thabiti wa mafanikio na maendeleo ya nchin
Watanzania wameaswa kuitunza
na kuidumisha amani iliyopo kwani ndiyo msingi thabiti wa mafanikio na maendeleo
ya nchin
Wakizungumza na KALI ZOTE BLOG kwa nyakati tofauti baadhi ya
viongozi wa dini wa madhehebu mbalimbali mjini Shinyanga wamesema moja ya wajibu wa viongozi wa dini ni
kuwahamasisha waumini wao kuitunza,na kidumisha amani kupitia mafundisho kwenye nyumba za ibada
ili kuifanya nchi iendelee kuwa huru na salama
Wamesema uhuru wa watu,maendeleo,usalama
wa nchi na hatua zozote za mafanikio
vinategemea zaidi hali ya amani na utulivu
-----
Kwa upande wake muinjilisti
marko Daud wa kanisa la k.k.k.t Ebeneza Shinyanga mjini amesema msingi wa
kuimarisha na kudumisha amani inahitaji kila mwananchi kutii,na kuheshimu
mamlaka na sheria za nchi zilizopo,
kwani hata mafundisho na vitabu vitakatifu vinaelekeza hivyo.
---.
Wamesema watanzania wanapaswa kujifunza kutokana na mifano ya
nchi zenye vita,mizozo na migogoro ambapo
hazina maendeleo kiuchumi,kisiasa,kiutaaduni na kijamii,lakini pia watu wake hawana uhuru
wala amani.
Post a Comment