Header Ads

Juhudi za kukabiliana na vitendo vya ukeketaji zinazofanywa na wadau mbalimbali katika wilaya ya Tarime mkoani Mara



Juhudi za kukabiliana na vitendo vya ukeketaji zinazofanywa na wadau mbalimbali katika wilaya ya Tarime mkoani Mara 


Image result for picha ya shinyanga


Juhudi za kukabiliana na vitendo vya ukeketaji zinazofanywa na wadau mbalimbali katika wilaya ya Tarime mkoani Mara zimekuwa hazifikii malengo yaliyokusudia kutokana na mila hizo kuchukuliwa kama chanzo cha kujiingizia kipato.

Hayo yamebainishwa na mkurugenzi wa Shirika la ATFGM  Bw. VARELIAN MGANI ambaye shirika lake linatkeleza mradi wa kuzia vitendo vya ukeketaji kwa watoto wa kike katika wilaya hiyo.

Akizungumza katika kikao cha kubadilishana uzoefu na shirika la AGAPE la mjini Shinyanga ambalo linaendesha mradi wa kuzuia mimba na ndoa za utotoni Bw.MGANI amebainisha kuwa juhudi wanazozifanya za kuzuia ukeketaji zinakumbana na changamoto kubwa kutoka kwa viongozi wa kimila na Mangariba ambao wanalipwa ujira mkubwa kutokana na kzi hiyo.

Kwa upande wake mwanasheria wa shirika hilo BI. IRENE THOMAS amezitaja  changamoto  nyingine zinazowakabili ni kukosa ushirikiano kwa jamii katika kesi zinawakabili wanaojiusisha na vitendo vya ukeketaji   ikiwemo zile zinazohusu ndoa za mimba za utotoni..


Shirika la ATFGM la mkoani MARA ambalo liko chini ya kanisa Katoliki  na shirika la AGAPE ala mjini Shinyanga kwa pamoja yanatekeleza miradi mbalimbali yenye lengo la kumkomboa motto wa kike kwa kuhakikisha yanaondoa vikwazo vyote vinavyomfanya asipige hatua.

No comments