Header Ads

mtaa wa dome atalini msim huu wa mvua

Wakazi wa mtaa wa Dome kata ya Ndembezi katika Manispaa ya Shinyanga wametakiwa kuweka mazingira yao katika hali ya usafi,ili kuchukua tahadhari ya  magonjwa ya mlipuko katika kipindi hiki cha masika.





Akizungumza na redio faraja  ofisini kwake  mwenyekiti wa serikali ya mtaa wa Dome  Solomon Nalinga amesema katika kipindi hiki ambacho mvua za masika zimeanza kunyesha,ni vyema wananchi kuchukua tahadhari dhidi ya magonjwa ya mlipuko .

                                         --
Mwenyekiti huyo amesema kiongozi bila kuwa na utashi wa kazi ni chanzo cha kutengeneza mazingira magumu kiusalama,na kwamba Ili Nchi  iweze kupiga hatua ya mafanikio na maendeleo  viongozi na watendaji  kuanzia ngazi ya serikali za mitaa wanapaswa kuwa na utashi wa kazi na uwajibikaji kwa  maslahi ya Jamii
Ametoa wito kwa Jamii hususani vijana kufanya kazi kwa bidii badala ya kuzurura,kutumia vilevi na kufanya uhalifu.


                           
Bwana NALINGA ametumia fursa hiyo kukumbusha wajibu wa  viongozi wa  serikali za mitaa,vijiji na vitongoji kushirikiana na serikali kuu  kutengeneza mazingira salama ya Jamii ili ipende  kufanya kazi na shughuli  halali kwa lengo la kujipatia kipato,ikiwa ni Pamoja na kudhibiti uhalifu

                                                                                  

No comments