Header Ads

wana kijiji wa seseko kulia machozi ya dam




wana kijiji wa seseko kulia machozi ya dam

Image result for picha ya barabara





Baadhi ya wakazi wa kijiji cha Seseko kilichopo katika Kata ya Mwamalili Manispaa ya Shinyanga wamewalalamikia viongozi kushindwa kuweka mgawanyo sawa wa  huduma  za kijamii,kwani huduma nyingi   zimeelekezwa zaidi katika kijiji Jirani cha Mwamalili

Wakizungumza na redio faraja fm stereo kwa nyakati tofauti wamesema kijiji cha Seseko kinakabiliwa na ukosefu wa huduma za kijamii ikiwemo maji,barabara,na zahanati hali inayowakatisha tamaa na kuwafanya wakose imani kwa serikali yao.
 Wamelalamia pia  kutokamilika   ujenzi wa Jengo la Zahanati  ambapo ni  muda mrefu sasa tangu kuanza kwa ujenzi wake,hali inayowalazimu kufuata huduma za afya katika vijiji Jirani



Kwa upande wake mwenyekiti wa serikali ya kijiji cha Seseko EZEKIEL MABULA amekiri kuwepo changamoto hizo na kusema kuwa tayari wamefikisha kwenye uongozi wa ngazi za Juu akiwemo diwani,na kwamba wananchi waendelee kushirikiana kuishinikiza serikali ili waweze kupata ufumbuzi wa kero hizo.
                                                
Wananchi hao wameiomba serikali kukisikia kilio chao na kisha kutafuta ufumbuzi ili kuwawezesha kupata huduma hizo ambazo ni stahiki kijamii.


No comments