Header Ads

TANZANIA YA ZIDI KUPINGA ATUA ZAIDI


TANZANIA YA ZIDI KUPIGA ATUA ZAIDI




Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na watoto Ummy Mwalimu mapema leo amekutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Qatar Abdullah Al Maadadi ofisini kwake na kuzungumza kuhusu masuala mbalimbali yanayohusu sekta ya afya.
 Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akizungumza na Balozi wa Qatar nchini Tanzania Abdullah Al Maadadi.


Katika mazungumzo yao yaliyofanyika ofisi za wizara hiyo Jijini Dar es salaam Waziri Mwalimu amesema kuwa Qatar imeonesha nia ya kuendelea kushirikiana na Tanzania kwaajili ya kutatua matatizo mbalimbali yaliyopo kwenye sekta ya afya hasa maeneo ambayo bado hayajafikiwa na huduma za uhakika za afya


Amesema katika mazungumzo na balozi huyo wamekubaliana kuanza mchakato wa kuwa na makubaliano ya mahusiano rasmi kwa kusaini hati ya makubaliano ambayo yataweka wazi maeneo ya ushirikiano kati ya Qatar na Tanzania.

Kwa upande wa Qatar wameonyesha nia ya kuisaidia nchi katika kutoa vifaa tiba kwaajili ya hospitali na kwa sasa tayari wizara hiyo imepokea magari 10 ya wagonjwa kutoka Qatar na taratibu za kuyatoa bandarini zinakamilishwa na zitapelekwa katika halmashauri mbalimbali ambazo hazina magari.





Kwa upande wake Balozi wa Qatar Abdullah Al Maadadi amekubali kuisaidia Tanzania katika kuleta vifaa tiba na kufanya ujenzi kwa baadhi ya wilaya nchini ambazo mapato yake bado ni kidogo hayawezi kukidhi gharama za ujenzi wa hospitali na vituo vya afya sambamba na kuleta wataalamu wa matibabu ya upasuaji wa moyo wataalamu ambao watashirikiana na wataalamu wa taasisi ya moyo ya Jakaya Kikwete ya

No comments