alikiba ajipanga baada ya kusaini mkataba na kampuni ya Sony
alikiba ajipanga
baada ya kusaini mkataba na kampuni ya Sony
baada ya kusaini mkataba na kampuni ya Sony
Kama ulidhani Alikiba atapotea kwenye ramani ya muziki baada ya
kusaini mkataba na kampuni ya Sony Music kama ilivyowahi kuwatokea
baadhi ya wasanii wa Afrika – imekula kwako, mwenyewe amefunguka.
Hitmaker huyo wa ‘Aje’ amekiambia kipindi cha 255 cha Clouds FM,
Alhamisi hii kuwa hawezi kukaa kimya zaidi ya miezi mitatu bila ya
kuachia nyimbo mpya kitu ambacho amedai kitamfanya awe juu zaidi.
“Nimejiandaa vizuri na pindi unapokuwa unasaini kitu, ina maana kuwa
umekubaliana na kila kitu, kwa hiyo mimi pia ninamatakwa yangu na hata
wao pia wanamatakwa yao. Kwa hiyo kitu ambacho kipo hapo ni kwenda na
agreement. Mimi siwezi kukaa muda zaidi ya miezi tatu bila kutoa ngoma
na huo ndio mkataba wangu jinsi unavyosema,” alisema Alikiba.
Muimbaji huyo alifanikiwa kusaini mkataba na kampuni hiyo mwezi Mei
mwaka huu na tayari ameshafanikiwa kuachia wimbo mmoja mpaka sasa akiwa
chini ya kampuni hiyo.
Post a Comment