Header Ads

Vikundi vya ujasiriamali vimeshauriwa kuondoa itikadi za kivyama na kidini ilikuweza kupiga hatua katika kuleta maendeleo

Vikundi vya ujasiriamali vimeshauriwa kuondoa itikadi za kivyama na kidini ilikuweza kupiga hatua katika kuleta maendeleo 

Image result for picha ya vikundi vya ujasilia mali


Vikundi vya ujasiriamali vimeshauriwa kuondoa itikadi za kivyama na kidini ilikuweza kupiga hatua katika kuleta maendeleo 
.
Akifunga warsha fupi ya kusoma mapato ya kikundi cha ujasiriamali ambacho kinajishughulisha na ulimaji wa mbogamboga katika kijiji cha Nhelegani manispaa ya shinyanga mwenyekiti wa kijiji hicho Seni Shija amewaomba wanakikundi kuondoa itikadi za kisiasa na imani za kidini ili kuondoa tofauti katika kuleta maendeleo.


Mwanzo wakati kikundi hicho kikisoma risala yake mbele ya mgeni kimesema kuwa kikundi kinakabiliwa na changamoto kama ukosefu wa elimu ya ujasiriamali kwa wakulima, upungufu wa mtaji kwa wakulima na vitendea kazi kwa ujumla.


Diwani wa kata ya kizumbi bwana Ruben Kitinya ambaye alikuwa ndiye mgeni rasmi amewapongeza wanakikundi hao kwa hatua ambayo wameweza kufikia hivi sasa na kuweza kutoa ahadi ya kushirikiana nao ,ikiwa pamoja na kuleta wataalamu wa elimu ya ujasiriamali na kufanya marekebisho katika visima vya maji ambavyo ni vibovu.


Naye mwenyekiti wa kikundi hicho ndugu Mbogo Mustafa Sombi ameisihi serikali ya awamu ya tano na jamii kwa ujumla kuvikumbuka vikundi vidogovidogo vya ujasiriamali pindi vinapohitaji msaada.




No comments