Joka mwenye sumu kali zaidi duniani huenda akawa jibu la kupatikana dawa ya kupunguza uchungu kwa wanawake duniani.
Joka mwenye sumu
kali zaidi duniani huenda akawa jibu la kupatikana dawa ya kupunguza
uchungu kwa wanawake duniani. Hii ni kwa mujibu ya wanasayansi.
Joka anayejulikana
kama 'Blue Coral' ndiye mwenye sumu kali zaidi na hupatikana zaizi
Kusini Mashariki mwa Bara Asia. Utafiti mpya uliochapishwa kwenye jarida
la afya la Toxin umepata joka huyo huwalenga maadui wake ambao
husababisha uchungu kwa binadamu.
Wanasayansi wanasema huenda
sumu hii ikatumika kutengeneza dawa ya uchungu. Baadhi ya wanyama ambao
sumu yao imetumika kutengeneza dawa ni pamoja na konokono wa baharini na
bui bui wa sumu.
Wanasayansi sasa wanataka joka huyu kuhifadhiwa
hususan baada ya maeneo mengi anakopatikana kugeuzwa kuwa mashamba ya
michikichi. Wanasayansi walifanya utafiti wao katika nchi za China,
Singapore na Marekani.
Watafiti wanasema japo kwa mwanadamu nyoka huwa adui, lakini wakati huu huenda akawa suluhu la matatizo mengi ya kiafya.
Post a Comment