Rais Magufuli ateua makatibu tawala
Rais Dkt. John Magufuli leo amemteua, Ado Mapunda kuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara
Taarifa ya Ikulu Jijini Dar es Salaam imesema Ado Mapunda anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Benedict Ole Kuyan ambaye amestaafu.
Pia, Rais Magufuli amemteua Tixon Nzunda kuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Rukwa.
Tixon Nzunda anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Symthies Pangisa ambaye amestaafu.
Tarehe ya kuapishwa kwa Makatibu Tawala wa Mikoa walioteuliwa itatangazwa baadaye
Post a Comment