Header Ads

alubino mkoa shinyanga waomba ulinzi

                      
 alubino mkoa shinyanga waomba  ulinzi 
Image result for picha ya shinyanga

Baadhi ya watoto wenye ualbino wanaolelewa katika kituo cha Buhangija mjini Shinyanga wameitaka serikali kuweka utaratibu wa kuwachukulia hatua viongozi wa maeneo yanakotokea mauaji ya watu wenye ualbino,kama njia ya kuwashinikiza kuweka mikakati ya kudhibiti mauaji hayo katika maeneo yao.

Wakizungumza na radio faraja katika kituo hicho watoto hao wamesema haiwezekazi wauaji watoke maeneo ya mbali bila kuwepo ushiriki wa watu wa karibu hali ambayo ingeweza kudhibitiwa kama viongozi wa maeneo husika wangeweka mikakati ya kuwalinda watu wenye ualbino waliopo katika maeneo yao.

Watoto hao pia wameiomba serikali kwa kushirikiana na wadau kuendelea kutoa elimu kwa jamii kuhusu watu maana ya ualbino ili kuondoa imani potofu ambazo zimejengeka miongoni mwa jamii kuwa viungo vyao vinaweza kusaidia kupata utajiri.

Kituo cha watoto wenye mahitaji maalum cha Buhangija,hivi sasa kinalea watoto wenye ualbino zaidi ya 200 ambao wamelazimika kuzikimbia familia zao kwa hofu ya kuuawa na watu wanaotafuta viuongo vyao.


No comments