Header Ads

kilicho jili kwenye kona ya soka hapo jana

kilicho jili kwenye kona ya soka hapo jana
Wachezaji wa Morocco
Michuano ya kombe la Afrika kwa wachezaji wa Ligi za Ndani ( CHAN) imehitimishwa Jumapili kwa ushindi wa wenyeji Morocco waliofanikiwa kulinyanyua taji la michuano hiyo kufuatia ushindi wa mabao 4-0 dhidi ya Nigeria.
Mchezaji wa Morocco Zakaria Hadraf alifanikiwa kupachika wavuni bao la kwanza muda mfupi kabla ya kipindi cha mapumziko huku mchezaji wa Nigeria Peter Eneji Moses akitimuliwa uwanjani baada ya kupewa kadi ya pili ya njano muda mfupi baad ya bao hilo.
Walid El Karti na Hadraf - katika bao lake la pili - waliipatia Morocco uongozi katika mechi hiyo kufikia dakika sitini.
Kampeni hiyo ilikamilishwa kwa bao la Ayoub El Kaabi, aliyegonga chuma mara mbili , na kufanikiwa kulifunga bao lake la tisa katika mashindano hayo ya wachezaji wa nyumbani wa timu za Afrika.
Nafasi ya kwanza ya Morocco ilikuja kunako dakika tatu za mechi wakati Walid El Karti aliposukuma tobwe katika eneo la karibuna lango kuu.
Wenyeji hao walidhani wameshafunga bao lao la kwanza katika dakika ya nne alipoisakata ngozi , kwa bahati mbaya naibu refa akanyanyua bendera akidai kiki hiyo ilisukumwa vibaya kabla ya kumfikia mshambuliaji huyo.
El Kaabi akasukuma hedi na kipa wa Nigeria Oladele Ajiboye ilibidi aokoe matobwe mawili kabla ya shinikizo la Morocco kujipa.
Kwa ukubwa Nigeria ilitegemea pasi ndefu kwa mashambulio yao na Anas Zniti wa Morocco hakuwana kibarua kikubwa kuokoa kabla ya muda wamapumziko.
Dakika mbili baada ya kipindi cha mpumziko Peter Eneji Moses alitimuliwa uwanjani baada ya kupewa kadi ya pili ya njano kwa mchezo m'baya dhidi ya Mohammed Nahiri.
Morocco ikaongeza bao la pili kunako dakika sitina wakati kiki ya El Kaabi ilipogonga chuma na kurudi nyuma kumwezesha El Haddad kusukuma kwa mara ya pili tobwe ambalo lilimfanya Ajboye asue sue na kumpa nafasi El Karti kusukuma kwa urahisi hedi ya nguvu ndani ya wavu.


Baada ya kuwepo kwa sintofahamu ya Cameroon kuwa wenyeji wa fainali za AFCON mwaka 2019 michuano ambayo inayotarajiwa kuanza June saba hadi Julai saba, kutokana na kutokuwepo kwa kimiundombinu mizuri na maswala ya uchumi kuweza kuandaa michuano hiyo , CAF ililazimika kufanya uchunguzi wa maandali zi hayo.
Baada ya CAF kumaliza kufanya uchunguzi hatimaye wametoa ruhusu kwa Cameroon kuendelea kufanya maandalizi kwa ajili ya michuano hiyo baada ya timu ya maafisa wa CAF kuridhishwa na maandalizi yanayoendelea nchini humo.
Juniour Binyam ni mwenyekiti wa kamati ya masuala ya habari wa CAF amethibitisha hilo na kusema kwamba CAF kwa sasa hawana mashaka juu ya maandalizi ya michuano hiyo na wanaona hadi kufika wakati huo Cameroon watakuwa tayari.
Inatajwa moja ya sababu kubwa iliyokuwa inatoa mashaka kwa CAF kuto waamini sana Cameroon ni kutokana na ongezeko la timu kutoka 16 kwenda hadi 24 jambo ambalo ilidhaniwa inaweza kuwa sumbua Cameroon lakini wanaonekana wanaweza kukabiliana nalo.
,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,
CAF yapitisha Cameroon mwenyeji mashindano ya Afcon 2019
Watford ilifunga mabao matatu ya dakika za lala salama kushinda mechi ya kwanza ya mkufunzi Javi Gracia dhidi ya Chelsea ,ushindi unaompatia shinikizo kali mwenzake wa Chelsea Antonio Conte.
Chelsea ilicheza takriban saa moja ikiwa na wachezaji 10 baada ya Tiemoue Bakayoko kupewa kadi nyekundu baada ya kucheza visivyo hatua ilioipatia Watford fursa ya kufunga mabao manne.
The Hornets ambao walikuwa wamepata ushindi mmoja kati ya mechi 12 walizocheza waliongoza kwa utata baada ya Gerard Deulofue kujiangusha kwa urahisi kufuatia kabiliano la kipa Thibaut Courtois huku Troy Deeney akifunga mkwaju wa penalti.
Chelsea iliomuingiza Olivier Giroud kwa mechi yake ya kwanza katika kipindi cha pili ilisawazisha wakati nyota wao Eden Hazard alipofunga bao zuri akiwa miguu 25 kutoka kwa lango.
Lakini dakika mbili baadaye ,Daryl Janmaat alifunga bao zuri wakati alipochenga kutoka wingi ya kulia na kucheza moja mbili na Robert Pereyra akawachenga mabeki wengine kabla ya kufunga na mguu wake wa kushoto.
Deulofeu aliongeza bao lake la pili wakati alipotamba na mpira na kushambulia kabla ya mpira kumpiga beki Gary Cahill na kuingia.
Watford sasa wako pointi sita juu ya eneo la kushushwa daraja.Gracia ambaye alichukua mahala pake marco Silva mwezi uliopita aliambia bbc Sport: Ulikuwa ushindi mkubwa na mechi nzuri, Nawapongeza wachezaji wangu.Tulicheza mechi nzuri , tukawasukuma sana.
''Mechi ilibailika baada ya kadi nyekundu kutolewa lakini nadhani tulicheza vyema. Chel;sea ni klabu kubwa sana , na timu kubwa''.
,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,
Fa Cup

Ratiba ya raundi ya tano ya kombe la Fa Kwa wanawake nchini England imetoka bingwa mtetezi Manchester City waanza kwa kusafiri kwenda kucheza na Birminghama City.
Mabingwa mara 14, wa michuano hiyo klabu ya Arsenal wao watakuwa wenyeji wa klabu ya Millwall, Chelsea watacheza na timu ya Doncaster Rovers Belles.
Michezo ya raundi ya tano ya kombe la FA, ambayo imebakiza jumla ya vilabu 16 itachezwa jumapili ya Februari 18.
Ratiba kamili ya michuano hiyo ni kama ifuatavyo
Arsenal v Millwall Lionesses
Cardiff City v Charlton
Lewes v Everton
Sunderland v Aston Villa
Chichester City v Liverpool
Birmingham City v Manchester City
Chelsea v Doncaster Rovers Belles
Durham v Plymouth Argyle or Leicester City

No comments