Header Ads

Ukubwa wa uume unategemea vitu kama kiwango cha mhemuko

Related image

Ukubwa wa uume unategemea vitu kama kiwango cha mhemuko, muda, hali ya hewa na unashiriki tendo la ndoa mara ngapi.
Si wanawake pekee ambao huwa bize kuona wanakuwa na maumbile mazuri na kwamba wanakuwa ni wenye kuvutia muda wote.
Ni kawaida kukuta chumbani kwa mwanamke vipodozi vingi vya kila namna na ukakuta mafuta ya aina moja tu kwenye chumba cha mwanaume.
Wapo wanaume wachache sana ambao wamebarikiwa kuwa na uume mkubwa kwa asili. Aina ya maisha unayoamua kuishi yanaweza kuathiri ukubwa na uimara wa uume wako.
Kwahiyo ikiwa una shaka kidogo juu ya ukubwa wa uume wako fanya mambo 8 yafuatayo kuongeza ukubwa wa uume kwa asili.
Mwanamke yeye huwa na uke wenye urefu wa inch 4 ingawa unaweza kuongezeka ukubwa kutegemea na namna anavyoandaliwa au mwanaume mwenyewe alivyo.
Kwa watu wazima, wastani wa ukubwa wa uume uliosimama ni kati ya inch 3.9 mpaka 5.8. Wapo pia wanaume wachache ambao kwa asili wana uume wa ukubwa wa inch 7 au 8.
Uume unachukuliwa kuwa mdogo ikiwa uko chini ya inch 4 ukiwa umesimama. Usiwaze ukubwa wa uume ukiwa umelala.
Kuna wanaume wa aina mbili, kuna wale ambao uume ukiwa umelala huonekana ni mkubwa lakini uume utakaposimama hauwi mkubwa sana na kuna wale ambao uume ukiwa umelala uume wao unaonekana ni mdogo sana na ndiyo hao ukisimama unakuwa mkubwa zaidi hata ya wale ambao ukiwa umelala unaonekana ni mkubwa.
Hivyo ukiona uume wako umelala na unaonekana ni mdogo sana usiwaze, ni hali ya kawaida, unatakiwa uwaze ukiwa umesimama kabisa.
mbegu-za-maboga
Kanuni mhimu 10 ili kuongeza ukubwa wa uume kwa asili
1. Acha kuvuta sigara
Moshi na kemikali za kwenye sigara hujirundika kwenye mishipa ya damu (ateri). Hii ndiyo sababu uvutaji sigara una uhusiano mkubwa na ugonjwa wa moyo.
Usambazwaji mdogo wa damu kwenye ogani hizo mwilini husababisha ufanyaji kazi wa chini ya kiwango wa ogani husika.
Kumbuka uume umeundwa kwa mishipa mitupu ya damu, hakuna mfupa kwenye uume.
Kama damu haitembei kwa uhuru wote katika ogani kadhaa mwilini na kwenye mishipa ya damu kwa ujumla uume wako nao unaweza kuathirika ukubwa wake.
2. Fanya mazoezi ya viungo mara nyingi
Kutengeneza mishipa na kupunguza uzito isiwe ndiyo sababu pekee ya kwenda gym.
Kama unahitaji uume wenye afya au uume mrefu, unahitaji kujishughulisha na mazoezi ya viungo mara kwa mara ili kusafisha mishipa ya damu na hivyo kuongeza kiasi cha utiririkaji wa damu kwenda kwenye uume.
Kama uzito wako upo juu sana na ni mnene fanya mazoezi ya kukimbia (jogging) kila siku kwa mwezi mmoja mpaka miwili.
Kama uzito wako upo sahihi tu kwa mjibu wa urefu wako fanya sana mazoezi ya kuchuchumaa na kusimama.
Una chuchumaa na kusimama mara 25 mpaka 30, unaweza kupumzika dakika mbili unaendelea tena kuchuchumaa na kusimama hivyo hivyo unapumzika dakika 2 mpaka mizunguko (round) 5 kila siku.
3. Epuka vyakula vyenye mafuta sana
Kula kwa wingi vyakula vyenye mafuta sana hupelekea kuongezeka kwa uzito na unene na matokeo yake unaweza kupatwa na magonjwa ya moyo na kupungua kwa ukubwa wa uume.
Kutokutenga muda kwa ajili ya mazoezi huongeza kolesto katika ateri za damu na kupelekea kupungua kwa msukumo wa damu kwenda kwenye uume.
Kwahiyo acha kula kula vyakula feki (junk foods) ili uwe na uume wenye afya ya kutosha.
4. Kula sana matunda na mboga za majani
Kula sana mboga za majani na matunda yenye sifa kubwa ya kuondoa sumu na taka mwilini. Mazoea haya husaidia mwili kupigana na vijidudu nyemelezi na kuongeza afya katika ateri za damu.
Kwahiyo unaweza kuongeza kimo cha uume wako kwa kuamua kula mboga majani na matunda ili kuondoa sumu na taka nyingine zisizotakiwa mwilini.
5. Ondoa kitambi
Kuwa na kitambi au tumbo kubwa ni sababu inayofanya uume uonekane ni mdogo. Hata kama una uume mkubwa kwa asili ukianza tu kufuga kitambi uume utaanza kuonekana ni mdogo.
Kuondoa kitambi soma pia dondoo namba 2 hapo juu.
6. Punguza mawazo
Hamaki na mawazo mengi (stress) hupunguza ukubwa wa uume kwani mawazo hasi au stress inapozidi na kudumu kwa muda mrefu huondoa damu kutoka kwenye uume na kupelekea ugumu kwa ukuaji wake.
Pia woga au wasiwasi wa kutokumfikisha mwenza wako unapodumu muda mrefu ni sababu ya kuwa na uume mdogo.
7. Oga maji ya moto
Hali ya ubaridi sana hupelekea kupungua kwa ukubwa wa uume, kwahiyo kama unaishi sehemu yenye baridi sana jitahidi uwe unaoga maji ya moto kila mara au muda mchache kabla ya kwenda kushiriki tendo la ndoa ili kuuweka mwili wako ni wa moto ili kuongeza msukumo wa damu mwilini na kwenye uume kwa ujumla.
8. Shiriki tendo la ndoa mara nyingi
Kuna stori zinasema twiga hakuzaliwa na shingo ndefu namna hii kama anavyoonekana akiwa mkubwa, bali wanasema ile tabia yake ya kupenda kula majani ya juu ya miti ndiyo ikapelekea shingo yake ikarefuka!. Inawezekana kuna ukweli kidogo wa stori hizi.
Usinielewe vibaya wala usije ukasema huyu jamaa anahamasisha watu kufanya mapenzi! Hapana usiwe na haraka hivyo utanielewa tu ninachotaka kusema
Wanasayansi wa masuala ya mapenzi wanasema ikiwa mtu mzima hana msongo wowote wa mawazo (stress), ana afya nzuri tu ya kutosha na anakula vizuri basi anaweza kushiriki tendo la tendo kila baada ya masaa 24.
Angalia na umsome pia mwenza wako pia angalia umri wako, sababu kuna wanawake wengine kwa asili hawapendi kushiriki tendo la ndoa kila mara pia hatuwezi kusema mtu mwenye miaka 50 atakuwa na uwezo wa kushiriki tendo la ndoa kila mara kama mtu wa miaka 18 hadi 40 hivi.
Ni vigumu mtu anakaa mwenzi mzima mwingine miezi miwili mwingine anakaa miezi 6 bila kushiriki tendo la ndoa na utegemee utakuwa na uume mzuri na wenye afya.
Kama hushiriki tendo la ndoa kuna uwezekano mkubwa ukawa unapiga punyeto kitendo ambacho ni kibaya zaidi kwa afya ya uume wako.
Kwahiyo unaweza kushiriki mara 2 hadi 3 kwa wiki na unaposhiriki tuliza akili na upate muda wa kutosha siyo haraka haraka tu (short time).
9. Tafuta wa saizi yako
Ni ukweli uliowazi kwamba kamwe hatuwezi kuwa sawa kwa kila kitu. Kuna msemo wa wahenga pia unasema waacheni wafu wawazike wafu wenzao, kadharika hata katika suala hili la tendo la ndoa mwanaume ifike wakati uamini kwamba kuna wanawake wengine si saizi yako, wapo wanaume kwa ajili yao.
Hivyo jiangalie mwenyewe na umtafute mwenza ambaye anaendana na wewe.
Wakati mwingine unaweza kupata mwenza ambaye ni saizi yako lakini sababu ya mabadiliko ya kimwili na kihomoni inatokea naye anakuwa anakuzidi, ikikutokea hivi usimwache, njoo uonane na mimi zipo dawa za asili maalumu zinazoweza kurudisha uke katika umbo dogo na unaobana vizuri kama mwanzo.
Au utaona aibu tena! Kuna namna ya kuongea naye.
10. Tumia mitishamba ambayo haina madhara
Ndiyo mitishamba, kuna baadhi ya mitishamba inayoweza kurekebisha mzunguko na msukumo wa damu yako na hatimaye kuongeza ukubwa wa uume.
Uwe makini sana hapa kwani unaweza kusababisha hatari zaidi hapo baadaye ukienda kwa pupa.
Usitumie dawa zinazoahidi kukuongezea urefu au ukubwa sana wa uume bila kujuwa nini madhara yake hapo baadaye, epuka pia dawa zenye kamikali kwa ajili hiyo.
mbegu-za-maboga
Jambo la mhimu
Badala ya kuwa bize na ukubwa wa uume wako, jitahidi kutafuta G-spot ili uweze kumchezea mwenza wako katika maeneo yanayomsisimua zaidi. Kumchezea mwenza wako ni muhimu sana ili aweze kufikia kileleni mapema.
Kuna mwingine anaweza kusema huyu jamaa naye vipi na hizi habari za ukubwa wa uume? Na ukaanza kunishangaa.
Mimi naandika chochote ninachoona kinaweza kuwa msaada kwa msomaji wangu, inawezekana wewe una msumari wa inch 6 na unaposikia habari kama hizi unaanza kushangaa na kudhani kama ni jambo lisilotakiwa kuzungumzwa.
Hivyo lolote linaloathiri kazi za uume linaathiri pia utendaji kazi kwa ujumla wa mwanaume husika.
Image result for UUME

No comments