Header Ads

Waziri Mahiga alitoa wito huo jana jijini Dar es Salaam katika kikao cha Baraza la Wakimbizi Duniani (WRF),




WAZIRI wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dk Augustine Mahiga ametoa wito kwa jumuiya ya kimataifa kuisaidia Tanzania kutokana na mchango mkubwa wa kuwahudumia wakimbizi, ambao imekuwa ikiutoa kabla na baada ya uhuru, licha ya uchumi mdogo ilionao.
Waziri Mahiga alitoa wito huo jana jijini Dar es Salaam katika kikao cha Baraza la Wakimbizi Duniani (WRF), kinachofanyika kwa siku mbili kuanzia jana.
Mahiga alieleza kuwa Tanzania ilipokea wakimbizi kutoka Poland wakati wa Vita ya Pili ya Dunia na mwaka 1959 ilipokea wakimbizi kutoka nchi ya Rwanda.
Aidha, baada ya Uhuru, Tanzania imekuwa ikipokea wakimbizi mara kwa mara na wakati wa mauaji ya kimbari nchini Rwanda, Tanzania ilipokea wakimbizi wengi zaidi duniani.
Alisema athari zinazotokana na kupokea wakimbizi wengi ni nyingi na kubwa hivyo, ni jukumu la jumuiya ya kimataifa kuzisaidia nchi zenye wakimbizi wengi, hususan zile zenya uchumi mdogo.
Katika kikao hicho, Waziri Mahiga alitoa ufafanuzi kuhusu msimamo wa Serikali ya Tanzania kujitoa katika Mpango wa Kutafuta Suluhu ya Kudumu ya Tatizo la Wakimbizi Duniani (CRRF).

No comments