Header Ads

Ajiua kisa wivu kwa mke wake


Image result for poison


Mwanaume mmoja mwenye umri wa miaka 43, Nicholas Wambua anayeishi katika eneo la 
Pipe Line Mjini Nairobi nchini Kenya, amejiua kwa kunywa sumu baada ya kumuhisi mkewe
 akimsaliti.

Mwanaume huyo ambaye alikuwa akifanya biashara ya mitumba katika eneo hilo, amefanya 
tukio hilo asubuhi ya Jumapili hii huku akiaacha ujumbe kwa watu wake wa karibu wamwambie 
mke wake huyo awaangalie watoto.

“Aliniambia ankwenda mbali na kuniomba nimwambie mama Sharon awaangalie watoto wake 
kwa ajili yake, ahtukujua akimaanisha kifo”, amesema Bi. Tabitha Bernad ambaye ni mkwe wa marehemu Wambua.
Mkwe wake huyo ameendelea kwa kusema kwamba mara nyingi marehemu alikuwa 
akimlalamikia kuwa mke wake ana tabia ya kuleta wanaume tofauti tofauti nyumbani kwao 
na kulala nao, iliniumiza kwa kweli lakini hatukupata muda wakuzungumza zaidi”, amesema 
Bi. Tabitha ambaye pia ni mkwe wa marehemu.

No comments