Header Ads

matokeo yote ya michezo ya kimataifa

Eliud Kipchoge wa Kenya ameshinda mbio ndefu za London Marathon kwa mara ya tatu. Alishinda katika mwaka wa 2015 na 2016
UK London Marathon 2018 | Gewinner Eliud Kipchoge und Vivian Cheruiyot aus Kenia (picture-alliance/Xinhua/R. Washbrooke)
Bingwa  wa  Olimpiki Eliud Kipchoge  ameshinda  taji  lake  la  tatu  la mbio ndefu marathon mjini  London  jana  Jumapili  na  kukamilisha ushindi  mara  mbili  wa  Wakenya  baada  ya  Vivian Cheruiyot kushinda   mbio  hizo  kwa  upande  wa  wanawake.
Kipchoge mwenye  umri  wa  miaka  33, alimshinda  Muithiopia  Tola Shura pamoja  na  Mo Farah  wa  Uingereza  na  kushinda  mbio  zake  za tatu  za  London Marathon  kwa  kutumia  muda  wa  masaa  2 dakika 4  na  sekunde  17, akimaliza  zaidi  ya  nusu  dakika  mbele  ya Kitata na Mo Farah  akiwa  wa  tatu  kwa  kutumia  masaa  2  dakika 21  na  sekunde 40.

Bayern Munich yaisubiri Real Madrid

Bayern yaisubiri  kwa  hamu  Real Madrid  katika  mtanange wa Champions League  wa kulipiza  kisasi.
Deutschland FC bayern München (imago/kolbert-press)
Kikosi hatari cha Bayern Munich
Champions League  inarejea  uwanjani  tena  kesho  na  keshokutwa Jumatano katika  awamu  ya  nusu  fainali, ambapo  klabu  kutoka ligi  nne  kubwa  za  Ulaya  zinawakilishwa. Kwa  mara  ya  kwanza tangu  mwaka 1981, timu  kutoka Uhispania , Real Madrid  England Liverpool, Italia  Roma  na  Ujerumani  Bayern Munich zinakuwa  timu nne  za  mwisho  katika  kinyang'anyiro  hicho cha  juu  cha  vilabu barani  Ulaya.

FC Kolon yachungulia daraja la pili

Hakuna jicho lililokosa  machozi  jana  mjini  Kolon wakati  FC Kolon ilipotumbukia  katika shimo la  kushuka  daraja  ...  wakati Hamburg SV yapata  matumaini  kwa  mbali  ya  kubakia  katika  Bundesliga.
1. Bundesliga | 1. FC Koeln v FC Schalke 04 (2:2) (picture-alliance/dpa/F. Gambarini)
Schalke 04  imeweka  mguu  mmoja  katika  michuano  ya Champions League  msimu  ujao wakati  FC Kolon  iko katika  ukingo wa  kushuka  daraja  baada  ya  sare  ya  mabo  2-2  jana  Jumapili. Wachezaji  pamoja  na  mashabiki  wa FC Kolon  macho yalimiminika machozi kuiona  timu  yao  ikiporomoja  licha  ya  kufanya juhudi  za ziada  kwa  kupata  ushindi  muhimu  jana.
Kolon walihitaji  kupata ushindi  jana  ili  kuweka  hai  matumaini  yao  ya  kubakia  katika daraja  la  kwanza lakini  mabao  ya  haraka  haraka  mnamo  kipindi cha  kwanza ya Breel  Embolo  na  Yevhen Konoplyanka yakiwakatisha  tamaa  , licha  ya  kupigana  kufa  na  kupona  na kukomboa  mabao  hayoMarcel Risse ndie  aliyefunga  bao  la kukomboa  la  FC Kolon  jana.

Arsene Wenger kuachia ngazi mwishoni mwa msimu

Makocha wa timu za ligi kuu ya England Premier League pamoja na wachezaji wa zamani wamemmiminia sifa kocha wa  Arsenal London Arene Wenger Ijumaa (20.04.2018) baada ya kutangaza atajiuzulu kuifunza timu hiyo.
FA-Cup Finale - FC Arsenal - FC Chelsea | Arsene Wenger (picture-alliance/Offside/M. Atkins)
 Wenger  mwenye  umri  wa  miaka 68 alishinda mataji  matatu  ya Premier League  na  vikombe  saba  vya  kombe  la  FA  katika  kipindi  cha miaka  22  akiwa  katika  uongozi  wa  timu  ya  Arsenal lakini  misimu  ya  hivi karibuni  imeamsha hali  ya  kutoridhika miongoni  mwa  mashabiki wakati klabu  hiyo  ilishindwa  kupambana  kuwania  taji  la  ligi

Schalke yawika mbele ya Dortmund

Ulikuwa mtanange uliosubiriwa na wengi mwishoni mwa wiki na sio tu kwa sababu ya utani wa tangu jadi wa timu hizo mbili, bali pia katika harakati za kutafuta nafasi ya Champions League. Schalke ikaizaba BVB 2-0
1. Bundesliga 30. Spieltag | FC Schalke 04 - Borussia Dortmund | Jubel Schalke (Getty Images/Bongarts/A. Grimm)
Schalke waliwazaba Borussia Dortmund mabao mawili na kujiimarisha katika nafasi ya pili ya msimamo wa Bundesliga. Hiyo bila shaka na hatua kubwa katika matumaini ya kupata tikiti ya moja kwa moja ya kucheza Champions League. Ushindi huo uliwapa nafasi ya kupumua kidogo maana sasa wana pengo la pointi nane kati yao na nambari tano RB Leipzig huku zikisalia mechi nne msimu kukamilika
kichapo hicho cha kwanza cha derby kwa Dprtmund tangu Septemba 2014 kimeiteremsha timu hiyo katika nafasi ya nne, nyuma ya Bayer Leverkusen na tofauti ya mabao. BVB iko nyuma ya Schalke na pengo la pointi nne na nne mbele ya Leipzig ambao walitoka sare ya bao moja kwa moja na Werder Bremen katika mechi nyingine ya jana.


Bayern mabingwa tena Bundesliga

Bayern Munich  yanyakua rasmi  ubingwa  wake  wa  sita  mfululizo katika  Bundesliga ,  Borussia  Dortmund yajisahihisha  na kuimarisha  nafasi  yake  ya  kucheza  Ulaya.
Fußball Bundesliga FC Augsburg - FC Bayern (Imago/kolbert-press/C. Kolbert)
Bayern Munich  imetia  kibindoni taji  lake  la  28 la  Bundesliga  wiki hii  baada  ya  kutawazwa  tena  kwa  mara  ya  sita  mfululizo  kuwa mabingwa  siku  ya  Jumamosi  baada  ya  kuikandika  Augsburg kwa  mabao  4-1.  Bayern  imedhihirisha  kwamba  wao  ni  washindi wasioshindia  katika  Bundesliga.


F1: Ricciardo aibuka mshindi nchini China

Katika mashindano ya magari ya Formula One, dereva Daniel Ricciardo wa timu ya Red Bull aliibuka mshindi wa mashindano ya Grand Prix ya China, ikiwa ni wa sita katika taaluma yake ya mashindano hayo
Formel 1 Großer Preis von China | Sieger Daniel Ricciardo (Getty Images/L. Baron)
Muasutralia huyo alichukua usukani katika mzunguko wa 45 baada ya kumpiku dereva wa Mercedes Valtteri Bottas. Bottas alimaliza katika nafasi ya pili huku Kimi Raikkonen wa Ferrari akipanda jukwaani katika nafasi ya tatu.
Mjerumani Sebastian Vettel ambaye ameshinda mikondo miwili ya kwanza msimu huu, alimaliza katika nafasi ya nane baada ya kuanza mashindano hayo akiwa katika nafasi ya kwanza. Pia aligongana na dereva wa Red Bull Max Verstappen na hivyo akapoteza nafasi kadhaa. Vettel bado anaongoza msimamo wa ubingwa wa dunia msimu huu akiwa na pointi 54, baada ya mikondo mitatu.
Lewis Hamilton, bingwa mara nne wa dunia na ambaye anatetea taji hilo, alimaliza katika nafasi ya nne na mpaka sasa ana pointi 43. Bottas ana pointi 40 katika nafasi ya tatu kabla ya mkondo ujao wa Azerbaijan.

Manchester City wabeba ubingwa wa England

Nchini England, Manchester City walitangazwa jana kuwa washindi wa Premier League baada ya nambari mbili Manchester United kuduwazwa  katika uwanja wa nyumbani na Westbromwich Albion bao 1 -0.
UEFA Championsleague | Manchester City v FC Basel (Reuters/A. Yates)
Wiki moja baada ya City kuzabwa 3-2 na United na kupoteza nafasi ya kutwaa ubingwa dhidi ya mahasimu hao wakali, ni West Brom inayochungulia kaburi la kushushwa ngazi ambayo iliwasaidia City kuanza sherehe za mapema za kunyakua taji hilo rasmi.
Ligue 1
Na nchini Ufaransa, Paris Saint Germain imejiunga na Manchester City ya England na Bayern Munich ya Ujerumani katika sherehe za ubingwa wa ligi. PSG walinyakuwa taji la Ufaransa jana kwa kuwazaba mabingwa watetezi Monaco mabao 7-1. Ushindi huo mkubwa ulidhihirisha pengo kubwa lilipo kati ya timu hizo mbili msimu huu. Ni taji la tano la tano al PSG katika misimu sita na la saba kwa jumla. PSG wako mbele ya nambari mbili Monaco kwa pengo la pointi 17 wakati kukiwa na mechi tano zilizosalia msimu huu.

Charlie nani? Mwendesha baiskeli mwanafunzi ashinda dhahabu Madola

Si hata mashabiki wa mbio za baiskeli waliwahi kumsikia Charlie Tanfield mwaka mmoja uliopita, lakini sasa Mwingereza huyo kijana ni bingwa wa michezo ya Jumuiya ya Madola, akiweka rekodi ya muda mrefu.
Australien 2018 Commonwealth Games 2018 | Charlie Tanfield (Reuters/P. Childs)
Charlie Tanfield akisherehekea baada ya ushindi katika mbio za mwendeshaji mmoja mmoja za mita 4000 huko Anna Meares velodrome - Gold Coast, Australia, Aprili 6, 2018.
Kimsingi mwanafunzi huyo anaesomea uhandisi wa umekanika, ambaye bado ni mwanagenzi, kwa namna fulani alikwepa nadhari ya wakuu wa chama cha waendesha baiskeli cha Uingereza hadi hivi karibuni -- lakini hawezi kupuuzwa tena.
Tanfield alipata ushindi katika fainali ya mbio za mita 4,000 katika uwanja wa Anna Meares Veladrome mjini Brisbane siku ya Ijumaa, na kuongeza medali ya dhahabu juu ya ile ya fedha alioipta saa 24 kabla ya hapo.





No comments