Header Ads

jipu moja kutubuliwa






Waziri wa Kilimo Mhe. Dkt Charles Tizeba amemuagiza Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Mhandisi Methew Mtigumwe, kusitisha mkataba wa kazi wa Mkurugenzi wa Bodi ya Korosho Tanzania Ndg. Hassan Jarufo.

Waziri Tizeba ametoa agizo hilo kwa katibu mkuu wa wizara hiyo jana jioni wakati leo akizungumza na wanahabari ofisini kwake mjini Dodoma ikiwa ni muda mchache mara baada ya kumalizika kwa hafla ya uwekaji  jiwe la msingi la ujenzi wa maghala na vihenge vya kisasa.
Mhe. Dkt Tizeba amesema uamzi wa kumsimamisha kazi  Mkurugenzi huyo, umekuja baada ya kuangalia mwenendo wa Ndg. Jarufo na kutafakari jinsi zao la Korosho linavyoendeshwa, ikiwa ni pamoja na kutoridhishwa na upatikanaji wa viuwatilifu kwa wakati.
Mkataba wa Jarufo umesitishwa kuanzia Aprili 21 na kwa mujibu wa Waziri Tizeba  alisema ndani ya muda mfupi Wizara ya kilimo itamtangaza Kaimu Mkurugenzi wa Bodi hiyo ili kuchukua nafasi hiyo na kuendeleza kusimamia sekta hiyo.
Aidha Mh. Tizeba ameongeza kuwa hatua kama hizo  serikali inazichukua lengo ikiwa ni kuhakikisha kuwa wadau wakubwa wa Korosho ambao ni wakulima wanaendelea kunufaika na zao hilo.
nandi afanya kitu cha ajabu angalia video hapa chini sylas tv

No comments