Header Ads

Tetesi za soka Ulaya Jumatano 25.04.2018

Luis Enrique

Arsenal inaamini inaweza kumshawishi aliyekuwa mkufunzi wa Barcelona Luis Enrique kuchukua mahala pake Arsene Wenger kama meneja wake.
Mkuu wa uhusiano katika klabu hiyo hiyo Rail Sanllehi alifanya kazi na Enrique katika klabu ya Barcelona.. (Mirror)
Mkufunzi wa zamani wa Chelsea Carlo Ancelotti, ambaye ni mkufunzi mwengine anayepigiwa upatu kumrithi Wenger amepewa kazi ya kuifunza timu ya taifa ya Italy.(Times - subscription required)
Image captionArsene Wenger
Mwenyekiti wa zamani wa Arsenal Peter Hill-Wood, ambaye amemuajiri Wenger mwaka 1996, amesema kuwa ni wakati kwamba mkufunzi huyo anafaa kuondoka. (Star)
Manchester City haina mpango wa kumuuza beki John Stones, 23, na raia huyo wa Uingereza yuko katika mipango ya mkufunzi Pep Guardiola. (Telegraph)
IniestaHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionIniesta
Guardiola anataka kushirikiana tena na kiungo wa kati wa Barcelona Andres Iniesta katika klabu ya Manchester City.
Mchezaji huyo wa Uhispania mwenye umri wa miaka 33 pia amehusishwa na klabu ya ligi ya kwanza nchini Ufaransa PSG mbali na kuelekea China. (AS)
Danny Rose
Image captionDanny Rose
Manchester United italazimika kutoa kitita cha £40m pamoja na beki wa Uingereza mwenye umri wa miaka 22 ili kuweza kumununua beki mwenza wa Uingereza na Tottenham Danny Rose, 27, kutoka Tottenham.(Sun)
Mbali na Rose, mkufunzi wa Manchester United Jose Mourinho anataka kumsaini beki wa kulia mwisho wa msimu huu. (Guardian)
Real Madrid italenga kumsajili mshambuliaji wa Bayern Munich Robert Lewandowski, 29,
Real Madrid italenga kumsajili mshambuliaji wa Bayern Munich Robert Lewandowski, 29, mwisho wa msimu huu kama suluhu ya muda mfupi huku wakiendelea kusaka saini ya mshambuliaji wa Tottenham Harry Kane, 24. (Sun)
Leicester inapanga kumsajili beki wa kulia wa Porto Ricardo Pereira, 24. Mchezaji huyo wa Ureno ana kipengee cha £36m kwa yeye kuondoka katika klabu hiyo (Mirror)
John TerryHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Beki wa zamani wa Chelsea na Uingereza John Terry, 37, anaweza kuongeza kandarasi yake na klabu hiyo hadi mwisho wa msimu huu (Talksport)
MorataHaki miliki ya pichaREX FEATURES
Washindi wa ligi ya mabingwa nchini Uingereza Wolves wanataka kumsajili beki wa Manchester City Eliaquim Mangala, 27, na hawatakuwa na tatizo lolote kumlipa raia huyo wa Ufaransa mshahara wa £85,000 kwa wiki. (Sun)
Tottenham imeanza mazungumzo na beki wa timu ya vijana nchini Uingereza Kyle Walker-Peters, 21. (ESPN)
West Ham itampatia beki wa Ireland Declan Rice, 19, mkataba wa muda mrefu . (Evening Standard)
Chelsea haitamuuza mshambuliaji wake wa Uhispania Alvaro Morata, 25, ama kiungo wa kati wa Ufaransa Tiemoue Bakayoko, 23, hadi pale watakapotaka kuondoka Stamford Bridge.. (Telegraph)
Mchezo wa kiwango cha kipekee wa Mohamed Salah uliisaidia Liverpool kuchukua udhibiti wa nusu fainali ya kombe la vilabu bingwa Ulaya-lakini mabao 2 ya dakika za lala salama ya Roma yaliipatia timu hiyo ahueni katika duru ya pili ya kombe hilo.
Liverpool ambao pia walifanikiwa kufika fainali ya 2007, waliipita safu ya ulinzi ya Roma bila pingamizi na kufunga mara tano katika dakika 68 za kipindi cha kwanza na cha pili katika uwanja wa Anfield.
Salah ambaye kwa sasa amefunga mabao 43 tangu ahamie Liverpool kutoka Roma alifunga mabao mawili na kutoa usaidizi wa mabao mawili.

Mohammed Salah akifunga bao lake la pili dhidi ya RomaHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionMohammed Salah akifunga bao lake la pili dhidi ya Roma
Aliuficha mpira katika kona ya goli kabla ya kumfunga tena kwa ustadi kipa Alisson kwa bao lake la pili.
Salah baadaye alipata mpira akatamba kabla ya kumpatia Sadio Mane pasi murua na kufanya mambo kuwa 3-0, kabla ya kutoa pasi nyengine kama hiyo kwa mshambuliaji Robert Firminio aliyefunga bao la nne.
Robert Firmino akimkumbatia Salah baada ya kufunga bao lakeHaki miliki ya pichaPA
Liverpool baadaye ilikuwa timu ya pili kufunga mabao matano katika mechi ya nusu fainali ya kombe la vilabu bingwa Ulaya wakati Firmino alipofunga kwa kichwa kona iliopigwa na James Milner.
Huku timu yake ikiongoza 5-0 baada ya dakika 68, Mkufunzi wa Liverpool Jurgen Klopp alimuondoa Salah na Roma ikajipatia fursa katika mechi ya marudio wiki ijayo katika uwanja wa Stadio Olimpico.
Kwanza Eden Dzeko aliifungia timu yake bao la kwanza kutoka kwa pasi ya Radja Nainggolan na baadaye Diego Perotti alifunga mkwaju wa penalti baada ya Milner kuunawa mpira katika eneo hatari.
Mashabiki wa Liverpool hawakuwanywa nyuma katika kuishabikia timu yaoHaki miliki ya pichaREUTERS
Image captionMashabiki wa Liverpool hawakuwanywa nyuma katika kuishabikia timu yao
Sasa Roma itahitajika kutumia kila mbinu ili kushinda 3-0 nyumbani Italy ili kusonga katika fainali ya kombe hilo.
Wiki mbili zilizopita Roma iliwashangaza mabingwa wa Uhispania Barcelona kwa kuwalaza 3-0 baada ya Barcelona kuicharaza timu hiyo 4-1 katika duru ya kwanza.
kiungo wa kati wa Liverpool Alex Oxlaide-Chamberlain alitolewa uwanjani kwa machela baada ya kupata jereha.Haki miliki ya pichaREUTERS
Mchezo bora katika mechi hiyo Mo SalahHaki miliki ya pichaEPA
Image captionMchezo bora katika mechi hiyo Mo Salah
Iwapo watafanikiwa kuilaza Liverpool nyumbani basi wataingia katika fainali dhidi ya Bayern Munich ama Real Madrid ambao wanakutana Jumatano kwa mechi nyengine ya nusu fainali.
Mbali na mabao mawili yaliofungwa na Roma katika kipindi cha pili cha mechi kiungo wa kati wa Liverpool Alex Oxlaide-Chamberlain alitolewa uwanjani kwa machela baada ya kupata jereha.
Kocha Jurgen Klopp anasema kuwa huenda kiungo huyo alipata jeraha 'baya sana'.
Kiungo wa kati wa zamani wa Ufaransa Henri Michel ambaye alikuwa mkufunzi wa mataifa manane wakati wa ukufunzi wake wa miaka 30 amefariki akiwa na umri wa miaka 70.
Aliichezea Ufaransa mara 58 na kuwafunza kutoka 1984 to 1988.
Michel aliiongoza Ufaransa, Cameroon, Morocco, Tunisia na Ivory Coast katika kombe la dunia na pia alikuwa mkufunzi wa timu za mataifa ya United Arab Emirates, Equatorial Guinea na Kenya.
Michel alishinda mataji matatu ya ligi alipoichezea klabu ya Nantes kwa kipindi cha miaka 16
Kazi yake ya ukufunzi ilianza na timu ya taifa ya Ufaransa ambayo ilishinda dhahabu katika michezo ya Olimpiki ya 1984 mjini Los Angeles .
Pia walifika katika nusu fainali ya kombe la dunia 1986.
Timu ya soka ya Kenya Harambee Stars
Image captionTimu ya soka ya Kenya Harambee Stars
Aliajiriwa kuifunza Cameroon 1994; aliifunza Morocco in 1995, UAE 2000, akawa mkufunzi wa Tunisia 2001; kabla ya kuwa mkufunzi wa Ivory 2004.
Michel alirudi nchini Morocco 2007 na baadaye akawa mkufunzi wa Equatorial Guinea na baadaye Kenya.
Alifanya kazi na klabu ya PSG mbali na vilabu vya Afrika ikiwemo Zamalek nchini Misri ,Raja Casablanca ya Morocco, mbali na Mamelodi Sundowns ya Afrika Kusini,

No comments