Header Ads

Maafisa watatu wakuu wa tume ya uchaguzi nchini Kenya (IEBC) akiwemo naibu mwenyekiti wamejiuzulu


Paul Kurgat (kushoto) Margaret Mwachanya (kati) na Consolata Nkatha

Maafisa watatu wakuu wa tume ya uchaguzi nchini Kenya (IEBC) akiwemo naibu mwenyekiti wamejiuzulu wakidai kutokuwa na imani na mwenyekiti wa tume hiyo, Wafula Chebukati.
Makamishna hao wamedai kuwa bodi hiyo imeshindwa kutimiza wajibu na imeeingiliwa na watu wengine.


Wakihutubia wanahabari jijini Nairobi, makamishna hao Consolata Nkatha, Paul Kurgat na Margaret Mwachanya wamedai kuwa Mwenyekiti wa IEBC, Wafula Chebukati ameshindwa kuiongoza tume hiyo na kudai kwamba tume hiyo imeingiliwa na watu kutoka nje wanaoshawishi jinsi inavyofanya kazi.

'Kwa muda murefu sasa, mwenyekiti ameshindwa kutoa muongozo wa utaratibu kwa wakati mgumu na anapohitajika kufanya hivo.
Katika taarifa yake hivi punde kwa waandishi wa habari, mwenyekiti wa tume hiyo ya IEBC - Wafula Chebukati amesema kwamba hakujakuwa na mawasiliano rasmi kuhusu kujiuzulu kwa makamishna hao watatu na kwamba amepata kusikia kuhusu taarifa hiyo kupitia vyombo vya habari nchini

                                                 MSUKUMA DARASA LA SABA

No comments