Header Ads

Nabii Tito ana ugonjwa wa akili...........apelekwe taasisi za magonjwa ya akili kwa ajili ya tiba



MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Dodoma imesema imejiridhisha kuwa mshitakiwa Onesmo Machibya (44), maarufu kama Nabii Tito ana ugonjwa wa akili hivyo apelekwe taasisi za magonjwa ya akili kwa ajili ya tiba.
Mahakama hiyo pia imemuachia huru katika kosa la kutaka kujiua baada ya kuthibitika kuwa alifanya hivyo kutokana na ugonjwa wa akili.
Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama hiyo, James Karayemaha ametoa uamuzi huo.
Hakimu Karayemaha amesema kutokana na taarifa ya uchunguzi wa akili wa mshitakiwa iliyopokelewa mahakamani hapo imethibitika kuwa Nabii Tito ni mgonjwa wa akili.
"Mahakama inamuachia huru katika kosa la kutaka kujiua na inatoa amri mshitakiwa kupelekwa hospitali ya wagonjwa wa akili na akishapona ataachiliwa huru aendelee na maisha yake," amesema Hakimu Karayemaha.
Nabii Tito kabla ya kukamatwa alikuwa akitoa mahubiri yanayoonekana kuhimiza ulevi na uasherati.
Alipandishwa kizimbani kwa mara ya kwanza Januari 29, mwaka huu na kusomewa mashtaka ya kujaribu kujiua ambapo alifanya jaribio la kujiua Januari 25, mwaka huu akiwa mahabusu, ambapo inadaiwa kwamba alijikatakata na wembe kwa lengo la kuyakatisha maisha yake.
Alipotakiwa kujibu mashtaka yanayomkabili, Nabii Tito awali alisema hakumbuki chochote kwa sababu yeye ni mgonjwa wa akili, lakini alipobanwa kwa mara nyingine, alisema ni kweli alitaka kujiua kwa sababu kuna sauti ndani ya kichwa chake iliyokuwa inamuelekeza kufanya kitendo hicho.
Janauri 23, mwaka huu, Kamanda wa Polisi mkoa wa Dodoma, Gilles Muroto alisema Nabii Tito alikamatwa baada ya kurekodi vipande vifupi vya video na picha vyenye maudhui ya kukashifu dini nyingine, na kuleta chuki dhidi ya watu wengine na kurusha mitandao ya kijamii, kinyume na kifungu cha sheria namba 129 cha kanuni ya adhabu sura ya 16 na marekebisho yake ya 2002.

msukuma dara la saba angalia

No comments