Header Ads

Nani atatamba kati ya Bayern Munich na Real Madrid?

Nani atatamba kati ya Bayern Munich na Real Madrid?

Bayern Munich kuchuana na Real Madrid uwanjani Allianz Arena katika mkondo wa kwanza wa nusu fainali ya Ligi ya Mabingwa
25.04.2018 Champions League: Bayern München gegen Real Madrid
25.04.2018 Fussball Champions League/ Hinspiel FC Bayern Muenchen gegen Real Madrid (picture-alliance/S. Simon)
Mtanange wa mkondo wa kwanza wa nusu fainali ya Ligi ya Mabingwa kati ya Bayern Munich na Real Madrid utakuwa mchuano wa kupigania pia ubabe wa soka la Ulaya. Kidumbwedumbwe hicho cha kwanza kati ya timu hizo mbili ni leo katika uga wa Allianz Arena.
Hii itakuwa mara ya 25 kwa timu hizo mbili kukutana katika soka la Ulaya, huku kila timu ikiwa imeshinda mara 11 na kutoka sare mara mbili. Leo usiku itakuwa mara ya saba kwa vilabu hivi kukutana katika nusu fainali. Katika mapambano yao yote, Real Madrid imefunga jumla ya mabao 37, Bayern mabao 36. 
Kocha wa Bayern Munich Jupp Heynckes amesema Real Madrid inapaswa kuwa na wasiwasi kuhusu Robert Lewandowski kama vile ambavyo Bayern Munich itakuwa inalenga kumdhibiti Cristiano Ronaldo.
Mabingwa hao wa Ujerumani wanawaalika Real katika mechi kali ya miamba ya Ulaya wakilenga kutwaa mataji matatu msimu huu. Bayern imethibitisha kuwa David Alaba hatashiriki mechi ya leo kutokana na jeraha la paja.
Macho wa Cristiano Ronaldo
Ronaldo amefunga mabao 42 katika mechi 39
Ronaldo amefunga mabao 42 katika mechi 39
Ronaldo amefunga mabao 42 katika mechi 39 wakati Lewandoswki ametikisa wavu mara 39 katika mechi 43. Mechi ya marudio ya nusu fainali kati ya timu hizo mbili itakuwa Mei mosi mjini Madrid.
Uchambuzi wa awali hasa umemlenga mshambuliaji wa Real Madrid Cristiano Ronaldo ambaye amefunga bao katika kila mechi zote 10 za Madrid katika Ligi ya Mabingwa msimu huu.
Amefunga mabao 9 katika mechi sita dhidi ya Bayern Munich.
Hata hivyo kocha wa Real Madrid Zinedine Zidane ameonya kuwa Bayern Munich wako imara wakati huu kuliko walipowabandua nje ya kinyang'anyiro hicho msimu uliopita.
Zidane amesema kuwa watahitaji kuonyesha uchezaji wa kiwango cha juu dhidi ya Bayern, huku akiongeza kuwa suala kuwa waliwaondoa katika robo fainali msimu uliopita halijalishi lolote wakati huu.
Hapo jana, Liverpool iliwachabanga Roma mabao matano kwa mawili katika mechi ya kusisimua iliyochezwa uwanjani Anfield. Nyota wa Liverpool Mohamed Salah alifungia timu yake mabao mawili miongoni mwa mabao hayo matano na kuonesha umahiri wake

Kocha Bayern asema Real AMdris wanapigika

Bayern Munich ilipoteza nafasi kadhaa katika kipigo chao cha magoli 2-1 nyumbani dhidi ya Real Madrid katika duru ya kwanza ya nusu fainali ya Champions League, lakini Kocha Jupp Heynckes amesema bado wana matumaini.
Fußball Bundesliga FC Augsburg - FC Bayern (picture-alliance/dpa/A. Gebert)
Bayern walipaswa kuongoza kwa magoli kadhaa katika kipindi cha kwanza kutokana na fursa walizokuwa nazo Thomas Mueller, Robert Lewandowski, Mats Himmel na Franl Ribery.
Lakini Wajerumani hao waliangushwa na umalizaji mbaya isivyo kawaida, uliowaruhusu mabingwa watetezi Real Madrid kuchomoka na ushindi na kuwaacha Bayern katika hatari ya kuondolewa mashindanoni na klabu ya Uhispania kwa msimu wa tano mfululizo.
"Hatukati tamaa," alisema Heynckes, aliyeiongoza Bayern katika ushindi wa mataji matatu mwaka 2013. " Unapotengezena nafasi nyingi dhidi ya timu kama Real basi hii ni ishara pia kwamba hasimu wako anapigika."
"Hatuna cha kupoteza na tutacheza kwa uhuru. Pengine zaidi ya tulivyocheza katika duru ya kwanza kwa sababu mchezo wetu haukuwa imara kama ambavyo tungependa."
UEFA Champions League Halbfinale | FC Bayern München - Real Madrid | TOR Madrid (Reuters/M. Rehle)
Real Madrid wakifunga goli lao la kwanza kupitia kwa Marcelo, katika uwanja wa Alllianz Arena mjini Munich, Aprili 25,2018.
Majeraha ya mapema yawaponza
Bayern ilipata matatizo ya mapema kutokana na majeraha kwa Arjen Robben na Jerome Boateng lakini waliendelea kupenya ngome ya Real kwa urahisi katika dakika 45 za kwanza, huku walinzi wa klabu hiyo ya Uhispania wakipambana na kasi ya Ribery na Lewandowski.
Lakini badala ya kuongezea kwenye goli la ufunguzi la Joshua Kimmich alilolipachika wavuni katika dakika ya 28, walikubali goli la kusawazisha dakika ya 44 kupitia mkwaju uliopigwa kwa ustadi na Marcelo, baada ya Dani Carvajal kuupiga mpira kwa kichwa na kuangukia karibu na eneo alilokuwa Marcelo.
Baadaye kosa la kiulinzi lililofanywa na Rafinha liliwaruhusu real kufunga bao la ushindi na kuiacha Bayern ikihitaji ushindi mjini Madrid wiki ijayo ili kusonga mbele katika hatua ya fainali.
"Simlaumu yeyote lakini operesheni zetu za ulinzi katika magoli yote zilikuwa mbaya," alisema Heynckes. Umalizaji wetu pia haukuwa mzuri. Hatukuwa na umakini kama kawaida 

No comments