Waumini wa dini ya kikristu wameaswa kusimama imara katika imani badala ya
Waumini wa dini ya kikristu wameaswa kusimama imara katika imani badala ya
Waumini wa dini ya
kikristu wameaswa kusimama imara katika imani badala ya kuyumba na kutetereka
kutokana na changamoto mbalimbali wanazokutana nazo.
Hayo yameelezwa
Jana na Paroko wa Parokia ya ngokolo Padri
Adolf Makandagu wakati akihubiri kwenye adhimisho la misa ya Jumapili
kwenye kanisa kuu la Mama mwenye Huruma ngokolo mjini Shinyanga.
Amesema tabu,shida,matatizo
na mahangaiko isiwe chanzo cha kutetereka kiimani, na badala yake wanapaswa
kusali kwa kumtumainia mungu,ili waweze
kuyashinda majaribu na mitihani iliyopo mbele yao.
Padre Makandagu
amesema wakristu wanapaswa kuwa
wavumilivu wenye kupenda kusoma biblia,kujifunza na kuyajua mafundiso ya mungu
hali ambayo itawasaidia kusimama katika imani thabiti nakufata yote ambayo yesu aliwataka wafanye wanafunzi wake.
Amewakumbusha waumini kuwa
wana wajibu wa kuwarithisha
watoto wao mila na desturi
zinazozingatia imani na maadili
ya kikristu,lakini pia umuhimu wa kusaidiana
na kuwaombea wengine wenye
mahangaiko badala ya kuwatenga na kuwabagua kutokana na madhaifu yao kwani watu wote nisawa
Post a Comment